Category: MCHANGANYIKO
TFF yaanza kuiharibu Ligi Kuu
ALIPOCHAGULIWA kuwa Rais wa Kwanza wa Shirikisho la Kandanda Tanzania (TFF), beki wa zamani wa kimataifa wa Yanga na Pan African, Leodgar Chillah Tenga alitarajiwa kuleta mapinduzi makubwa ya soka hapa nchini.
Kung’ang’ania sensa isusiwe ni upuuzi
Sensa ya idadi ya watu na makazi inafanyika kuanzia Jumapili wiki hii hadi Septemba 2, huku baadhi ya Watanzania wakiendelea kuipinga hadi dodoso la dini litakapojumuishwa. Viongozi mbalimbali wa Serikali hususan Wakuu wa Mikoa na Wilaya wamekuwa wakiwaomba viongozi wa kisiasa na kidini kuwataka waumini wao washiriki kikamilifu kuhesabiwa kwa sababu ni faida yao wenyewe na taifa letu.
Bunge lisiposema, wabunge watasema
Nimemsikiliza Naibu Spika Job Ndugai akilalamika kwamba nidhamu ya baadhi ya wabunge, hasa vijana si nzuri. Ndugai anarejea matukio kadhaa yaliyotokea wakati wa Mkutano wa Bunge ulioahirishwa wiki iliyopita. Alikwenda mbali zaidi kwa kukumbuka mambo yalivyo tangu kuanza kwa Bunge la Kumi. Analalamika kwamba asilimia zaidi ya 70 ya wabunge wa sasa ni wageni. Kuna vijana wengi ambao bado hawajazisoma na kuzitambua vema Kanuni za Kudumu za Bunge.
Buriani Mbogora, bado sisi tunahangaika na Malawi
Moyoni nina majonzi. Natumia neno hili kwa vile siamini macho yangu, lakini ndivyo ilivyo. Hili linatokana na kifo cha mwanahabari mwandamizi, Alfred Mbogora. Nilimwona Mbogora siku moja kabla ya kifo chake, lakini zamu hii hakuwa akifahamu kama nilifika kumjulia hali katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, lakini angalau alitikisa mkono na mguu nilipoingia wodini. Hii ilikuwa Ijumaa.
Mahakama imekalia haki yangu miaka 16
Mhariri wa JAMHURI nimevutiwa kwa kiwango kikubwa baada ya kusoma toleo lenu Na 39 la Agosti 14-20, 2012 lililoongozwa na habari yenye kichwa kisemacho ‘Majaji Vihiyo Watajwa’. Mara tu niliposoma habari hii, nikaona ni vyema nifunge safari na kuja hapo ofisini kwako nieleze kilio changu. Wengi wa majaji waliotajwa wameshiriki kwa namna moja au nyingine kukandamiza haki yangu.
Hongera Mkapa, Kikwete alijiandalia aibu ya Mahalu
Napata wakati mgumu. Napata shida jinsi ya kuanza makaha haya. Napata shida si kwa sababu nina maslahi binafsi, bali kwa sababu nakumbuka hadithi ya mwanafunzi aliyebeba upodo huku akijifunza kurusha mishale ya sumu. Hakuwa mahiri na hakujua jinsi ya kuvuta upinde. Kwa kicheko kikubwa, aliipaka sumu ncha ya mshale, upinde akauelekeza karibu na tumbo lake, kamba ya kurushia mshale ikatokea mbele yake.