Category: MCHANGANYIKO
Asante RC Mwambungu, Inspekta Anna
Septemba 28 ni siku ya pekee maishani mwangu. Ilikuwa ni siku mbili tu tangu niliposafiri na kufika Songea mkoani Ruvuma. Nilipanga katika hoteli iliyopo katikati ya mji iitwayo Safari Lodge.
Urais: Sumaye anena ya moyoni
Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye amesema, tofauti na wanasiasa wengine, yeye akiutaka urais hatasubiri kuoteshwa. Amesema wakati wa kugombea urais ukiwadia, na kama akitaka kuwania nafasi hiyo, hakuna kizuizi kwake.
Simba, Yanga haponi mtu
Wapenzi na mashabiki wa soka nchini wanasubiri kwa hamu kesho mtanange wa watani wa jadi – Wekundu wa Msimbazi, Simba Sports Club ya jijini na Dar es Salaam Young Africans (Yanga) yenye makao yake makuu mitaa ya Jangwani na Twiga, watakapopepetana kwenye Uwanja wa Taifa katika Ligi Kuu Vodacom Tanzania Bara.
Ukiwa mnafiki utaifaidi CCM
Wengi tumemsikia Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, akiwaambia wanachama waliokatwa majina kwenye vikao vya mchujo kwamba anayetaka kukihama chama hicho, ahame haraka. Amesema CCM haiwezi kufa, na akaongeza kwamba wanaodhani kuwa CCM itakufa, watatangulia kufa wao.
Hapendwi mtu UK, hata awe waziri
Tabia ya Waingereza kuzijua na kuzitetea haki zao, inanipa faraja kubwa sana wana-Jamhuri wenzangu. Watu wakubwa wamejikuta wanaanguka kwa mambo yanayotokana na kushindwa kuheshimu wadogo. Mfano wake ni Mnadhimu Mkuu wa Serikali, Andrew Mitchell, anayetota matatani kwa kuwaita polisi wanaoshika lindo kwenye Ofisi za Waziri Mkuu pale Downing Street kuwa ni “kajamba nani” tu.
Yah: Tujiulize, maendeleo yaondoe utamaduni wetu?
Wanangu, wakati wa ujana wetu kulikuwa na starehe nyingi ambazo leo nyie hamuwezi kuzifanya kwa gharama yoyote ile labda mjigeuze na kuomba kwa Mwenyezi Mungu miaka irudi nyuma na mpate nafasi ya kufaidi kama tulivyofaidi sisi.