JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Bajeti ya kodi za bia, soda haitufikishi popote

WIKI iliyopita Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa alitangaza bajeti ya mwaka 2012/2013. Nafahamu kuwa mpendwa msomaji umeishasoma mengi kuhusiana na bajeti hii. Kwa mantiki hiyo mimi sitajielekeza katika kuchambua nini kimeongezwa kodi au kupunguzizwa kodi kama ulivyo utamaduni wa makala nyingi.

Tunafahamu sote sasa kuwa bajeti hii ya shilingi trilioni 15 na ushehi hivi, imekuwa ya ujumla mno. Bajeti hii sikuiona kama inalenga kutatua tatizo la njaa, umeme, barabara mbovu, reli, viwanja vya ndege, elimu, afya au hata mahusiano ya jamii. Kiwango kilichotengwa nadiriki kukiita umwagiliaji wa matone (drip irrigation).

Hata Waziri Mgimwa aliyeisoma bajeti hii kwa mara ya kwanza maishani mwake, naamini hadi leo yupo kwenye mshangao. Hajasikia mshindo. Hakuna jipya lililotokana na tangazo lake la bajeti. Labda hizo Sh milioni 50 anazotarajia kupata kutokana na matajiri wenye kuweka majina yao kwenye magari binafsi. Kwa bahati mbaya ingetokea mimi ndiye Waziri wa Fedha, nchi hii ningeishitua mbavu.

Wabunge waibane Serikali bila woga

Wabunge jana walianza kujadili Bajeti ya Serikali ya mwaka 2012/2013. Kama ilivyotarajiwa, mjadala wa bajeti ya mwaka huu wa fedha ni mkali.Wiki iliyopita wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliitwa katika Kamati yao ambayo Mwenyekiti wake ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Juhudi za Lowassa kuihangaikia elimu zinapaswa kuungwa mkono

 

Naweza kumpenda au kumchukia sana Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, lakini hata iweje sitajizuia kumuunga mkono mtu yeyote akifanya jambo jema au lenye tija kwa taifa.

 

Siku chache zilizopita, Lowassa aliongoza harambee iliyokusanya Sh. milioni 530 kutoka kwa wadau wa maendeleo ya elimu – fedha ambazo Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho yeye mwenyewe ni mwanachama wake, kilichangia Sh. milioni 20.

 

Ije Jubilee nyingine ya malkia tushibe

Si mapumziko hata kidogo, maana ni sikukuu lakini waliofanya kazi wametoka na vinono. Wengi wataendelea kumwombea Mtukufu Malkia Elizabeth II adumu na serikali iendelee kuridhia maadhimisho ya sherehe zake.

Adui wa Waislamu ni utamaduni wa Kiarabu wa Ghuba

*Ukristo ama Uislamu na serikali si tatizo katu
Naomba nichangie hapa kama Mtanzania -na si kama Mwislamu au Mkristo au mpagani. Mosi, ni kweli kwamba kitabu cha yule padri Mzungu, Dkt. John Sivalon kinaleta shida sana mawazoni mwa watu. Lakini turejee kwenye ukweli wa kisomi, kwamba huwezi kuhitimisha jambo zito kwa kutumia chanzo kimoja.

Yah: Uzalendo uliondoka kama Ujamaa na Kujitegemea?

Wanangu, leo nimeamka nikiwa na siha njema kabisa na kufurahi kwamba sasa mmeanza kuyaona yale ambayo labda sisi watu tunaoonekana wazee, mnaweza kuyaangalia kwa kina na kuyatafutia ufumbuzi wa kina ili tuondoke hapa tulipo twende huko kulikokuwa kunatarajiwa na wengi.