JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Kila mmoja analalamika

 

Sifa mpya ya Watanzania sasa ni kulalamika. Malalamiko yameshamiri katika kaya, mitaa, ofisi, sehemu zote za kazi na kila mahali. Kinachosumbua zaidi ni kuona kuwa hakuna aliye tayari kuondoa malalamiko hayo hata kama mwenye dhima hiyo ni yeye mwenyewe.

 

Uhuru wa habari na magazeti kwa wote

Gazeti la JAMHURI ni miongoni mwa midomo, macho na masikio ya Watanzania na wadau wengine wa habari. Uhuru wa habari – ambao dunia yote inautangaza na kuuenzi kwa sasa – ni haki ya kila raia na chombo cha habari.

TFF yaanza kuiharibu Ligi Kuu

ALIPOCHAGULIWA kuwa Rais wa Kwanza wa Shirikisho la Kandanda Tanzania (TFF), beki wa zamani wa kimataifa wa Yanga na Pan African, Leodgar Chillah Tenga alitarajiwa kuleta mapinduzi makubwa ya soka hapa nchini.

Kung’ang’ania sensa isusiwe ni upuuzi

Sensa ya idadi ya watu na makazi inafanyika kuanzia Jumapili wiki hii hadi Septemba 2, huku baadhi ya Watanzania wakiendelea kuipinga hadi dodoso la dini litakapojumuishwa. Viongozi mbalimbali wa Serikali hususan Wakuu wa Mikoa na Wilaya wamekuwa wakiwaomba viongozi wa kisiasa na kidini kuwataka waumini wao washiriki kikamilifu kuhesabiwa kwa sababu ni faida yao wenyewe na taifa letu.

Bunge lisiposema, wabunge watasema

 

Nimemsikiliza Naibu Spika Job Ndugai akilalamika kwamba nidhamu ya baadhi ya wabunge, hasa vijana si nzuri. Ndugai anarejea matukio kadhaa yaliyotokea wakati wa Mkutano wa Bunge ulioahirishwa wiki iliyopita. Alikwenda mbali zaidi kwa kukumbuka mambo yalivyo tangu kuanza kwa Bunge la Kumi. Analalamika kwamba asilimia zaidi ya 70 ya wabunge wa sasa ni wageni. Kuna vijana wengi ambao bado hawajazisoma na kuzitambua vema Kanuni za Kudumu za Bunge.

Buriani Mbogora, bado sisi tunahangaika na Malawi

 

Moyoni nina majonzi. Natumia neno hili kwa vile siamini macho yangu, lakini ndivyo ilivyo. Hili linatokana na kifo cha mwanahabari mwandamizi, Alfred Mbogora. Nilimwona Mbogora siku moja kabla ya kifo chake, lakini zamu hii hakuwa akifahamu kama nilifika kumjulia hali katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, lakini angalau alitikisa mkono na mguu nilipoingia wodini. Hii ilikuwa Ijumaa.