Category: MCHANGANYIKO
Hapendwi mtu UK, hata awe waziri
Tabia ya Waingereza kuzijua na kuzitetea haki zao, inanipa faraja kubwa sana wana-Jamhuri wenzangu. Watu wakubwa wamejikuta wanaanguka kwa mambo yanayotokana na kushindwa kuheshimu wadogo. Mfano wake ni Mnadhimu Mkuu wa Serikali, Andrew Mitchell, anayetota matatani kwa kuwaita polisi wanaoshika lindo kwenye Ofisi za Waziri Mkuu pale Downing Street kuwa ni “kajamba nani” tu.
Yah: Tujiulize, maendeleo yaondoe utamaduni wetu?
Wanangu, wakati wa ujana wetu kulikuwa na starehe nyingi ambazo leo nyie hamuwezi kuzifanya kwa gharama yoyote ile labda mjigeuze na kuomba kwa Mwenyezi Mungu miaka irudi nyuma na mpate nafasi ya kufaidi kama tulivyofaidi sisi.
Ahadi hizi za Kikwete zinatekelezeka?
Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2010, mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, alitoa ahadi nyingi mno.
Kikwete apendelea familia yake CCM
*Ahakikisha wanne wa familia yake wanapita
*Naye akichaguliwa uenyekiti atakamilisha ‘The Kikwete 5’
*Mwanae mwingine ni Mjumbe Chipukizi Taifa
*NEC ijayo itakuwa ya Baba, Mama na Watoto (BMW)
Mjadala mkali umeibuliwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ukihusisha familia ya Kikwete kuwa na wagombea watano wa nafasi tofauti ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Tayari majina manne yameshapitishwa, huku jina la Rais Jakaya Kikwete likisubiriwa kuwa la tano wakati atakapojitokeza kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa CCM Taifa.
Siku ya Kujua: Nguzo ya maendeleo duniani
Maendeleo ya binadamu yamebaki kuwa mtihani mgumu unaosumbua vichwa vya wengi wanaoendesha Serikali, taasisi binafsi au kuajiriwa. Kila binadamu anafanya kazi kwa nia ya kujiletea maendeleo binafsi ili hatimaye maendeleo ya mtu mmoja mmoja yazae maendeleo ya taifa kwa ujumla.
Elimu iwajenge wanafunzi kujitegemea
Serikali ya hapa Uingereza inaandaa mabadiliko makubwa ya elimu amabko mfumo wa mitihani utakuwa tofauti. Lazima nasi Watanzania tujifunze kitu hapa kwa sababu tumekuwa na kasumba ya kubadili mfumo bila sababu zake kueleweka wazi.