JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Rooney kuipaisha Uingereza fainali za Kombe la Dunia

Mwanasoka wa kimataifa wa nchini Uingereza, Wayne Rooney, anayechezea klabu ya Manchester United, anatarajiwa kuongoza kikosi cha England dhidi ya San Marino katika mtanange wa kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia zitakazofanyika nchini Brazil, mwaka 2014.

Serikali iisaidie BFT kuwezesha mabondia

Michuano ya ngumi Afrika inatarajiwa kufanyika Casablanca, Morocco, baadaye mwezi huu, wakati Tanzania imeteua mabondia 13 watakaoiwakilisha huko, baada ya kuonesha uwezo mzuri katika mashindano ya Taifa yaliyofanyika Dar es Salaam, hivi karibuni.

Yanga yasumbua vichwa vya mashabiki

Wakati Wekundu wa Msimbazi, Simba Sports Club ya jijini ikifanya vizuri kwa kujikusanyia pointi nyingi mwanzoni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, mahasimu wao wakubwa zaidi, Dar es Salaam Young Africans (Yanga) yenye makao yake mitaa ya Jangwani na Twiga, imekuwa ikisuasua na kuzua maswali mengi kutoka kwa mashabiki wake.

Madaraka Nyerere azungumza

Juzi, tarehe 14 Oktoba 2012, tumetimiza miaka 13 tangu kufariki Mwalimu Julius Nyerere, kiongozi wa kwanza wa Tanganyika huru, na baadaye Tanzania.

Wasindikizaji Ligi Kuu Bara wajulikana

 

Wakati Simba Sports Club ikiendelea kuongoza Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara hadi mwishoni mwa wiki, timu za Toto African, Ruvu Shooting, Polisi Morogoro na Mgambo Shooting bado zinashindana mkiani zikionesha dalili za kuwa wasindikizaji msimu huu.

Akrama anavyoshutumiwa mechi ya Simba, Yanga

Jumatano iliyopita timu za Simba na Yanga zilishindwa kuoneshana ubabe, baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Kabla ya mchuano huo, Simba ilikuwa ikipewa nafasi kubwa ya kushinda hasa kwa vile iliingia uwanjani ikiwa imeshinda michezo yote minne ya awali, huku Yanga ikiwa imeshinda miwili na kufungwa mbili pia.