Category: MCHANGANYIKO
Migogoro imeiua Simba msimu huu
Hatimaye Mashindano ya Ligi Kuu ya Vodaco Tanzania Bara yamemalizika huku Klabu ya Simba ikiambulia kushika nafasi ya tatu, huku mtani wao wa jadi, Yanga ikitwaa ubingwa wa ligi hiyo, ikifuatiwa Azam FC iliyoshika nafasi ya pili.
Mwalimu Nyerere na usawa katika jamii
Taifa letu kwa sasa linapita kwenye misukosuko ya udini, ukabila, ukanda na utegemezi. Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, hakusita kamwe kukemea kwa nguvu zote utengano huo, na kusisitiza nchi kujitegemea.
Tumeirejesha JKT, sasa tuifufue Chipukizi
Wiki iliyopita nilizungumza na wabunge wawili-Martha Mlata na Wiliam Ngeleja, kwa nyakati tofauti. Hawa ni miongoni mwa wabunge waliokuwa ziarani China.
Nilimwuliza, Mlata ni mambo gani yamemvutia baada ya kuiona China . Kabla ya kujibu, uso wake ulionesha namna alivyopata shida ya “aanze kuzungumza lipi”. Aanze kuzungumzia flyovers alizoona, azungumzie kilimo au anieleze kuhusu uzalendo wa Wachina kwa Taifa lao.
Yah: Tuliangalie sakata la elimu kwa sasa [1]
Mwaka 1932 nilianza darasa la kwanza katika Shule ya Kati Bulongwa. Nilikuwa na miaka kumi na nne. Nilipata nafasi hiyo baada ya nenda rudi ya miaka miwili, mkono ulikuwa haufiki sikioni.
Tamasha la Siku ya Mkerewe kuanza Juni
Shirika la Kuboresha Mienendo na Desturi kwa Ustawi (KUMIDEU) katika Wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza, linashirikiana na wadau mbalimbali kuandaa tamasha la Siku ya Mkerewe.
Serikali inachekea udini, maadui wanalifahamu
Najua wengi wameandika mada hii. Ni karibu wiki sasa tangu kutokea kwa ugaidi kule Arusha. Wengi wameibuka na mijadala yenye kusisitiza kuwa kilichotokea Arusha ni mwendelezo wa udini. Baadhi wamefika mahali wanasema wazi kuwa Serikali imetunga majina ya watuhumiwa.