JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Yah: Litakuwa Taifa la watoto, wazee 

Nianze kwa kuwapongeza kutimiza miaka makumi kadhaa ya Muungano, yaani Muungano ambao leo mnadai kuwa una kero ambazo sisi wakati tukiungana tuliona siyo kero za Muungano bali ni chachu za Muungano, na ndizo zinazofanya utamu wa Muungano kuwapo.  Sina hakika,…

Nyalandu aweweseka siri kuvuja

*Aanza kuwasaka wabaya wake, awatisha Aprili 22, mwaka huu, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, akiwa na baadhi ya watendaji waandamizi wa Wizara hiyo mjini Dodoma, alitoa vitisho akiahidi kuwashughulikia wote aliodai kuwa wanavujisha siri za ofisi kwa watu…

Kipande abanwa Bandari

*Nguvu za ajabu alizokuwa nazo zaanza kuyeyuka, alalamika Kikwete hamsaidii
*Marafiki zake wamtaka asimsingizie Rais, wasema amejiharibia mwenyewe
*Ashinikizwa awarejeshe kazini aliowafukuza kibabe, wafanyakazi washangilia
*Aanza kuogopa kivuli chake, ajitolea ‘photocopy’, adai wanaomsaliti anao TPA
*Mtawa asema asihusishwe na Kipande, bandarini wasema JAMHURI mkombozi
*Mwakyembe aweweseka, adai Lowassa, Profesa Tibaijuka hawamtakii mema
Nguvu za ajabu alizokuwa nazo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Madeni Kipande (58), zimeanza kuyeyuka kwa kasi baada ya GazetiJAMHURI kuchapisha mfululizo maovu anayotenda kwa kutumia wadhifa wake.
Vyanzo vya kuaminika vilivyopo karibu na Kipande, vinasema kwa sasa ameacha kumwamini kila mtu na hasa baada ya JAMHURI kupata habari za ndani ya kikao alichokuwa anatamba kuwa amemng’oa Mkurugenzi wa Masoko, Francisca Muindi, kitu ambacho hakutarajia kuwa kingelifikia gazeti hili.

Yah: Tusichezee lugha yetu, wengine wanajuta

Wakati tunatawaliwa, wakoloni wote kwa awamu zao yaani Wajerumani, Waingereza na hata Wareno na Waarabu, wakati wakipita kwa biashara zao sisi Wazaramo na Wandengereko tulikuwa tunawasiliana kwa shida sana. Kuna wakati tulikuwa tunatumia lugha ya alama kuwasiliana. Baada ya kuanza…

NUKUU

Mwalimu Nyerere: Tudhibiti tofauti za maskini, matajiri “Tofauti kati ya watu maskini na watu matajiri zinaongezeka Tanzania. Inafaa tuwe macho. …lazima tuendelee kutumia Sheria za Nchi, na mipango mbalimbali ya Serikali, kuona kuwa tofauti hizi hazifikii kiasi cha kuhatarisha umoja…

Mwadui ni bora kuliko nyingine nchini – Julio

Kocha wa Timu  ya Soka  ya Mwadui ya mkoani Shinyanga, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, ametamba kwamba timu hiyo itakuwa bora katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara kuliko zote zinazoshiriki.

Akizungumza na JAMHURI hivi karibuni,  Julio amesema kuwa timu hiyo itatoa upinzani mkali kwa timu za Simba,  Yanga  na Azam FC.

“Simba na Yanga hakuna mpira pale bali kuna makelele, niliwahi kufundisha timu ya Kajumulo, sikuwahi kufungwa na Simba wala Yanga na hata sasa nikifanya usajili wangu hakuna timu ya kunifunga kati ya timu hizo,” amesema Julio na kuongeza: