JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Bodi ya Wakurugenzi TPA haina meno mbele ya Kipande

Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) haina meno mbele ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya hiyo, Madeni Kipande, baada ya kubainika kuwa maelekezo mengi anayopewa na Bodi anayapuuza.

Baada ya Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, kuunda Kamati ya Mbakileki kuchunguza kinachoendelea bandarini wakati wa uongozi wa Ephraem Mgawe, Kamati ilitoa mapendekezo ambayo bodi ilimwagiza Kipande kuyatekeleza, lakini zaidi ya asilimia 90 ya mapendekezo hayo ameyapuuza.

Nyalandu apangua ‘amri’ ya Nyerere

*Aagiza wataalamu wafungue mpaka wa Bologonja

*Watalii kutoka Kenya wataingia kiulaini Serengeti

*Watafaidi vivutio, kisha fedha zote zitaishia Kenya

Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, ameshakamilisha mipango ya kufungua mpaka wa Bologonja; jambo linalotajwa kuwa ni pigo kwa uchumi wa Taifa na kwa wadau wa tasnia ya utalii nchini.

Mpaka huo unaotenganisha Tanzania na Kenya, ulifungwa mwaka 1977 kwa amri ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, kwa kuzingatia maslahi mapana ya kiuchumi na kimazingira ya Taifa.

Taarifa zilizopatikana kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii zinasema tayari Nyalandu ameshawaagiza viongozi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) na wengine katika Wizara yake, kuhakikisha mpaka huo unafunguliwa.

Mkurugenzi  Mtendaji wa TTB, Aloyce Nzuki, ambaye Nyalandu amemwondoa kwenye nafasi hiyo, anatajwa kuwa mmoja wa watu waliopinga mpango huo kama ilivyokuwa kwa watangulizi wake. Upinzani huo unatajwa kuwa miongoni mwa sababu alizotumia Nyalandu kushinikiza Nzuki aondolewe.

Real Madrid kuivua ubingwa Bayern leo

Miamba minne ya soka barani Ulaya, wiki hii inajitupa tena katika viwanja viwili tofauti kucheza nusu fainali ya kuwania Kombe la Klabu Bingwa Ulaya (UEFA). Miamba hiyo ni mabingwa watetezi wa kombe hilo, vijana wa Pep Guardiola wa Bayern Munich,…

CCM inapohusishwa na kila kitu

Katika maisha ya jadi niliyoishi kijijini, kila kitu kilichotokea kilihusishwa na Mungu. Kama kuku hawakutaga mayai mengi kutokana na kutopewa chakula cha kutosha, watu walisema ni amri ya Mungu.

Kama mtu alikufa kwa ugonjwa kwa sababu ya kucheleweshwa kupelekwa hospitali, watu walisema ni amri ya Mungu. Na kama watoto walichezea moto ukaunguza nyumba, watu walisema ni amri ya Mungu.

Mipasho Bunge la Katiba ikomeshwe

Bunge Maalum la Katiba limeahirisha vikao vyake hadi Agosti mwaka huu, kupisha vikao vya Bunge la Bajeti vitakavyopokea na kujadili taarifa za mapato na matumizi ya Serikali ya Muungano kwa mwaka 2014/2015.

Bunge hilo kabla ya kuahirishwa Aprili 25, mwaka huu kwa takriban miezi miwili, yaani tangu Februari 18, mwaka huu wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba walikuwa katika vikao vizito, wakifanya mambo makuu mawili. Watanzania tumeshuhudia.

IGP Mangu dhibiti udhaifu huu

Katika siku za karibuni, Jeshi la Polisi Tanzania limechukua hatua mbalimbali za kujisafisha mbele ya umma. Ni baada ya kubaini kwamba wananchi wengi walikuwa hawaridhiki na utendaji wa chombo hiki cha dola.