JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Yanga, Simba ‘fowadi’ mbovu

Ikiwakilishwa na timu nne za Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club, Dar es Salaam Young Africans (Yanga), Azam FC zote za jijini na Mafunzo kutoka Zenji katika hatua za awali za michuano ya Kombe la Kagame, Tanzania ilipata fedheha kubwa katika mechi zilizochezwa siku ya kwanza na ya pili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mke wa Msekwa, wenzake wanavyotafuna nchi

*Kikao cha siku moja walipata Sh milioni 7

*Mjumbe mmoja asaini posho mara mbili

*Mkewe Mudhihir ambaye si mjumbe alipwa

 

Ufisadi unazidi kuwaandamana viongozi wa CCM. Safari hii, Mbunge wa Viti Maalumu, Anna Abdallah, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho pamoja na wajumbe wa Bodi hiyo, wanatuhumiwa kujilipa mamilioni ya shilingi. Ulaji huo umefichuliwa na Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Rose Kamili, katika hotuba yake ya makaridio ya mapato na matumizi ya mwaka wa fedha wa 2012/2013

 

BODI ZA MAZAO YA BIASHARA NA MAENDELEO YA KILIMO

Mheshimiwa Spika, kilimo cha mazao ya biashara hapa nchini kwa sasa kina changamoto nyingi. Changamoto hizo ni pamoja kukosa soko na bei za uhakika za mazao hayo.

Yah: Nahisi sasa kuwa ni mganga wa kienyeji

Tangu zamani dhana kwamba mtu mzee ndiye mchawi katika jamii, imejengeka sana miongoni mwa walio wengi wenye upeo mdogo wa kufikiri na kuiaminisha jamii yenye maadili mema kuwa na imani potofu kwa sisi wazee.

CCM ni kama wameitwa na chunusi

Mbunge wa Mbozi Magharibi, David Silinde (Chadema) mwanzoni mwa mkutano wa Bunge unaoendelea sasa, alizungumza maneno ya hekima.

 

Akieleza safari ya kifo cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) alifananisha hali hiyo na tajiri anayefilisika. Akasema tajiri anayefilisika huwa hajitambui, na kwamba akijitambua kuwa anafilisika, kamwe hatafilisika. Hatafilisika kwa sababu atajitahidi kutafuta mbinu za kujikwamua. Akasema kwa hali ya mambo ilivyo, CCM haijitambui kama inakufa, na kwa sababu hiyo, inakufa!

Yah: Haiwezekani Mtanzania abaguliwe ndani ya Tanzania

Wanangu, naamini mu bukheri wa afya na mnaendelea kufanya kazi kwa bidii kama tulivyokuwa tukifaya sisi wakati wa ujana na afya zetu.

Yah: Tulianza kusimama dede sasa tunabebwa.

Wanangu nianze kwa kuwapa kongole kwa kazi za kuliendeleza taifa ambalo linamkosi mkubwa na jambo linaloitwa maendeleo, linamkosi kwa sababu kwa kipindi cha miaka hamsini ya tangu kuzaliwa kwake bado linachechemea, kwa ufupi ndio kwanza linaanza kusimama dede ili lipige hatua ya kwanza lakini dalili zote za kushindwa zinajidhihirisha.