JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Kikwete apendelea familia yake CCM

 

*Ahakikisha wanne wa familia yake wanapita

*Naye akichaguliwa uenyekiti atakamilisha ‘The Kikwete 5’

*Mwanae mwingine ni Mjumbe Chipukizi Taifa

*NEC ijayo itakuwa ya Baba, Mama na Watoto (BMW)

 

Mjadala mkali umeibuliwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ukihusisha familia ya Kikwete kuwa na wagombea watano wa nafasi tofauti ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Tayari majina manne yameshapitishwa, huku jina la Rais Jakaya Kikwete likisubiriwa kuwa la tano wakati atakapojitokeza kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa CCM Taifa.

 

Siku ya Kujua: Nguzo ya maendeleo duniani

Maendeleo ya binadamu yamebaki kuwa mtihani mgumu unaosumbua vichwa vya wengi wanaoendesha Serikali, taasisi binafsi au kuajiriwa. Kila binadamu anafanya kazi kwa nia ya kujiletea maendeleo binafsi ili hatimaye maendeleo ya mtu mmoja mmoja yazae maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Elimu iwajenge wanafunzi kujitegemea

Serikali ya hapa Uingereza inaandaa mabadiliko makubwa ya elimu amabko mfumo wa mitihani utakuwa tofauti. Lazima nasi Watanzania tujifunze kitu hapa kwa sababu tumekuwa na kasumba ya kubadili mfumo bila sababu zake kueleweka wazi.

Yah: The big four The big poor, So what?

Wanangu poleni na uchovu wa mawazo. Sitaki kuwapa kongole ya kazi kwa sababu naomba nikiri wazi kuwa nyote ni wababaishaji na hamna lolote mnalofanya zaidi ya kuungaunnga kile tulichokifanya sisi kwa ujana wetu.

Makanisa mengi ni dalili ya kukata tamaa

Juzi nimesoma habari inayohusu utajiri wa kutisha, wa baadhi ya viongozi wa madhehebu ya kikristo. Viongozi wanaotajwa, wengi wao ni hawa wa madhehebu yanayoibuka na kusajiliwa kila siku. Nilifurahi kusoma habari hiyo kwa sababu imebeba kile ambacho mara zote nimekiamini.

Yanga ina jinamizi la saikolojia

Kila upande wa mabingwa wa kandanda Afrika Mashariki na Kati, Dar es Salaam Young Africans (Yanga) yenye makao yake makuu katika mitaa ya Jangwani na Twiga jijini, unaelekea kukabiliwa na jinamizi la kisaikolojia.