JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Mwenyekiti Musukuma apuuzwe

Magazeti kadhaa yameripoti kwamba Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Joseph Musukuma, amewaambia wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji cha Nyawilimilwa kilichopo Kata ya Kagu, kwamba hatakuwa tayari kupeleka maendeleo katika kata hiyo kwa sababu inaongozwa na Diwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Mashindano ya Miss Tanzania yafutwe

Wakati huu wa harakati za kutoa maoni ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni wakati mwafaka kutafakari kama mashindano ya ‘Miss Tanzania’ yanaikosea Tanzania.  Mwaka 1964 Serikali ilipiga marufuku mashindano hayo lakini yakaibuka kinyemela mwaka 1994 kwa mfano wa Azimio la Zanzibar, lililoibuka mwaka 1992 bila mwafaka wa kitaifa, na kuathiri Azimio la Arusha lililozaliwa mwaka 1967.

EfG inavyopinga ukatili kwa wanawake

Shirika lisilo la Serikali la Kuwezesha Wanawake Kibiashara (EfG) Tanzania, limekuwa mstari wa mbele kusaidia wafanyabiashara wasio katika sekta rasmi, ikiwa ni juhudi za kuinua nafasi zao katika nyanja mbalimbali ikiwemo ya kiuchumi.

Miaka 51 ya Uhuru, 50 ya Jamhuri: Tumekwama wapi?

Juzi Jumapili nchi yetu imetimiza miaka 51 ya Uhuru tangu tulipoupata Desemba 9, 1961 na mwaka mmoja baadaye ndhi yetu ikawa jamhuri. Kwa hiyo tumetimiza pia miaka 50 ya Jamhuri ingawa hili halitajwi sana.

Kituo cha Mabasi Ubungo: Mgodi wa mafisadi

*Hoja ya Mnyika yawekwa kapuni

Utangulizi

Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT) kilifunguliwa rasmi Desemba 6, 1999 pamoja na mambo mengine, uanzishwaji wa kituo hiki ulikuwa na madhumuni ya kutoa huduma kwa wasafiri pamoja na watumiaji wengine na pia kuongeza mapato ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Kikwete alivyowalilia Sharo Milionea, Mlopelo, Maganga

Rais Jakaya Kikwete, ameelezea kustushwa na kusikitishwa na vifo vya wasanii maarufu nchini, Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’, Khalid Mohamed ‘Mlopelo’ na John Stephano Maganga.