JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Ujasiriamali ni ajira kamili

Nilipokuwa muhula wa mwisho kumaliza masomo ya shahada yangu ya kwanza, siku moja niliingia katika mjadala mzito na mama yangu mzazi. Mama alikuwa akishusha pumzi kuona kuwa mwanaye sasa ninaelekea kukamilisha ngwe ya elimu ya juu. Mawazo na kiu yake kubwa ilikuwa ni kuona natafuta ajira mapema, kitu ambacho nilitofautiana naye na hivyo kuzusha malumbano ya kihoja na kimtazamo.

Yah: Kama Ningekuwa waziri wa kodi

Wanangu, hongereni kwa kuvuka mwaka uliopita na kuukaribisha mwaka mpya na mambo yaleyale ya mwaka jana kwa tofauti ya tarehe na mwaka, nawapa kongole kwa sababu baadhi yetu tukiingia mwaka mwingine tunajitengenezea malengo ambayo lazima yatekelezeke.

Serikali, Basata walivyomlilia Sajuki

Kifo cha msanii maarufu hapa nchini, Juma Kilowoko, maarufu kwa jina la Sajuki, kimeigusa Serikali na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), miongoni mwa wadau wa sanaa na Watanzania kwa jumla.

Taifa Stars rarua Ethiopia

Januari 11, mwaka huu, mashabiki wa soka na Watanzania kwa jumla wataelekeza macho na masikio yao mjini Adis Abab, Ethiopia, wakati Taifa Stars itakapojipima nguvu na wenyeji wao.

Kikwete chukua hatua nchi inameguka vipande

Wiki iliyopita yametokea maandamano mjini Mtwara. Maandamano haya kwa yeyote anayeyaangalia kwa jicho la kawaida yalikuwa na nia njema. Yalilenga kuwapa fursa Watanzania wenyeji wa Mkoa wa Mtwara, kueleza malalamiko yao na haja yao ya kupata faida ya gesi. Wanataka badala ya gesi kusafirishwa kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam bomba lisijengwe.

Kuna umuhimu wa wafanyabiashara ‘kunolewa bongo’

Hongera sana ndugu wasomaji wa JAMHURI kwa kuuanza Mwaka Mpya wa 2013. Wiki kadhaa huko nyuma tulichapisha makala katika safu hii iliyokuwa na makosa katika kichwa cha habari, hivyo kuleta usumbufu wa kimantiki kwenu wasomaji.

Kichwa hicho kilichokosewa kilisomeka hivi: “Wafanyabiashara wanapaswa “kuolewa bongo zao”. Tunapoanza Mwaka Mpya nimeona ni busara niirudie makala ile katika maana na dhana niliyoikusudia.