JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Ligi Kuu Bara isiwe ya Simba, Yanga

Mara nyingi ubingwa wa mashindano ya soka ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, umekuwa ukibebwa na Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club ya jijini na Dar es Salaam Young Africans (Yanga), yenye makao yake mitaa ya Jangwani na Twiga, kana kwamba timu nyingine hazina wachezaji mahiri wenye uwezo wa kushinda.

Yah: Jamani kama ningelikuwa mbunge

Wanangu mu hali gani, siku zote nawaandikia barua lakini siwaulizi hali zenu, mara zote huwaeleza siha yangu bila kujua siha zenu. Nimeona sitendi haki kwa kuwa kujua hali zenu ni jambo bora zaidi kuliko kuwafikishia ujumbe wangu, maana naweza kuwa nafikisha ujumbe katika uwanja wa makaburi ambako mmelazwa kutokana na ugumu wa maisha.

Kuta za ‘Oysterbay’ hazitazuia hasira za masikini

Sakata la usafirishaji gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam lilipoanza, sikusita kuunga mkono madai ya wana-Mtwara. Kuna kundi la viongozi na wananchi waliothubutu kupotosha ukweli wa madai ya wananchi hao.

FASIHI FASAHA

Tunakubali rushwa ni adui wa haki? (3)

Katika sehemu ya pili ya makala haya, nilionesha jitihada za Serikali katika kuzuia na kupambana na rushwa nchini, kwa kutunga sheria na kuunda vyombo vya kukabiliana na tatizo hilo.

Misaada hii ya udhalilishaji Afrika no!

Moja ya mambo ambayo Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, yatamfanya asisahaulike kwayo, ni kule kujiamini hata kuwakemea wakoloni na rafiki zao.

Waislamu wachinje, sisi tule nguruwe wetu

Wiki iliyopita niliandika makala juu ya usaliti wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, kwa yeye kuamua kuulisha umma uongo uliozaa madhara ya hali ya juu kwa wananchi wa Mtwara. Sitarudia nilichokiandika, ila niwashukuru wananchi na hasa wewe msomaji kwa mrejesho.

Nimepokea simu nyingi, ujumbe na barua pepe pengine kuliko wakati wowote tangu tuanzishe gazeti hili. Nawashukuru mno wasomaji kwa kueleza hisia zenu. Sitaweza kufafanua kila mmoja alisema nini, ila niseme karibu asilimia 95 ya waliowasiliana na mimi walinipongeza.

 

Sitanii, walinipongeza kwa kuamua kumfunga paka kengele. Hawakutarajia iwapo ningethubutu kumwambia Zitto kuwa katika hili hapana. Katika masuala ya nchi, siasa tuziweke kando. Alinichekesha msomaji mmoja aliyeniandikia hivi: “Kaka wengine wanatuchochea tupigane vita maana wanajua mambo yakiharibika kwetu watarudi kwao.”

 

Usiniulize ni nani mwenye uraia wa nchi mbili, ambaye hana uchungu na nchi yetu kiasi cha kutuchochea tupigane kisha arejee kwao. Ninalosema, gesi itunufaishe sote kama Watanzania. Nimemsikia Zitto ameanza tena uchochezi akidai Kigoma kuna mafuta, ila waelezwe watabaki na nini.


Sitanii, kichwa cha makala haya, kinasema: Waislamu wachinje, sisi tule nguruwe wetu. Nimelazimika kuandika makala haya baada ya kubaini sura ile ile ya upotoshaji katika jamii yetu. Mwanza kumeibuka kundi la watu wanaojiita Wakristo kuliko Waroma.

 

Kundi hili linashinikiza na kuhamasisha utengano katika jamii. Kundi hili limepeleka malalamiko kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Evarist Ndekillo, likidai Wakristo waruhusiwe kuchinja. Waziri wa Uhusiano wa Jamii, Stephen Wasira, amefika pale akajaribu kusuluhisha mgogoro huu, inaelekea ameshindwa.

 

Nikisoma katika mitandao naona wakubwa huko Mwanza wameanzisha hadi bucha zao. Wanachinja wenyewe na kuwauzia Wakristo wenzao. Nimejaribu kufuatilia chimbuko la mgogoro huu. Wanasema Waislamu wanawadharau kwa kula nguruwe.


Eti Waislamu wanataka hata maduka ya nguruwe yaliyopo katika mitaa yao yavunjwe kuepusha kukwaza imani yao. Hapo ndipo ninapopingana na Waislamu sawa na nilivyopingana na Wakristo. Katika utawala wa Awamu ya Pili ya Rais Ali Hassan Mwinyi, nchi yetu ilipata mgogoro kama huu.  Mzee Mwinyi alimaliza tatizo hili kwa busara ya hali ya juu.