JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

fasihi fasaha

Tunakubali rushwa ni adui wa haki? (4)

Ni miaka 17 sasa tangu Tume ya Kero ya Rushwa ilipotufahamisha mianya na sababu za kuwepo rushwa, wala rushwa na njia za kuitokomeza. Lakini kilio kikubwa cha madhara ya rushwa bado kinasikika kutoka kwa wananchi.

FIKRA YA HEKIMA

Tunahitaji rais dikteta mwenye uzalendo

Jumamosi iliyopita wakati jua likielekea kuchwea, nilihisi faraja kuandaa makala hii kutoa changamoto kwamba nchi yetu sasa inahitaji kuwa na rais dikteta lakini aliye mzalendo. Dikteta ni mtu anayetawala nchi kwa amri zake bila kushauriwa, au anayetaka analosema litekelezwe bila kupingwa, na mzalendo ni mtu anayependa nchi yake kiasi cha kuwa tayari kuifia.

Elimu imetushinda, sasa tujaribu ujinga

Wiki iliyopita nimesikiliza kwa umakini mkubwa mjadala uliokuwa unaendelea katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nimemsilikiza Mbunge wa Kuteuliwa rafiki yangu, James Mbatia, alivyokuwa aking’ang’ana na ‘Serikali Sikivu’ kuwaeleza kuwa mtaala unaofundishwa sasa unatupeleka shimoni.

Wanasiasa sasa waliteka Bunge

*Walitumia kujinyooshea mapito kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015

Bunge la Kumi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemalizika wiki iliyopita huku kwa kiasi kikubwa likionekana kugeuzwa kuwa jukwaa la siasa.


Wabunge kutoka vyama vya siasa, hususan Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameonekana kulitumia Bunge hilo kutafuta umaarufu wa kisiasa kwa wananchi. Wabunge kutoka katika vyama hivyo wameweka maslahi ya taifa pembeni na kukumbatia itikadi za vyama vyao.

RATIBA YA LIGI KUU TANZANIA BARA

Jumamosi Februari 9, 2013 Mtibwa Sugar Vs Azam FC Toto Africans Vs Coastal Union Kagera Sugar Vs Mgambo JKT TZ Prisons Vs African Lyon JKT Oljoro Vs Simba SC

Mambo muhimu Stars kucheza AFCON

Kocha wa timu ya soka ya taifa (Taifa Stars), Kim Poulsen, amesema kuwa haoni sababu itakayoizuia Tanzania kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2015.