Category: MCHANGANYIKO
Malinzi: Tuelekeze nguvu Morocco vs Taifa Stars
Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Kagera, Jamal Malinzi, amewataka Watanzania kuiunga mkono Taifa Stars iweze kushinda katika mchezo kuwania tiketi ya kufuzu Kombe la Dunia unaotarajiwa kufanyika Machi 24, mwaka huu.
Yah: Yawezekana maendeleo au tumelogwa?
Siamini kama mtu ambaye anayemwamini Mwenyezi Mungu anaweza kuamua, kwa mkono wake, kukatisha maisha ya mtumishi wa bwana kwa moyo safi na wa kijasiri. Haya naona ni maendeleo mengine ambayo enzi zetu hayakuwako, sielewi kama napaswa kuwapongeza au kuwalaumu kwa maendeleo hayo.
fasihi fasaha
Serikali ishughulikie vurugu za kidini
Naungana na Watanzania wenzangu kulaani mauaji ya viongozi wawili wa dini ya Kikiristo yaliyotokea mkoani Geita na mjini Zanzibar, hivi karibuni. Aidha, natoa mkono wa tanzia kwa familia, ndugu na waumini wa dini hizo.
FIKRA YA HEKIMA
Tumeruhusu kucheka na nyani shambani, tutavuna mabua
Ni wazi sasa maji yanaelekea kuuzidi unga! Nchi yetu iko katika hatari ya ‘kuvuna mabua’ kufuatia kasumba ya kutoa mwanya wa ‘kucheka na nyani shambani’. Serikali na vyombo vyake vya dola vitabaki kulaumiwa, kwa kushindwa kudhibiti mfululizo wa matukio ya kutisha yakiwamo mauaji ya watu kikatili.
Kasi yetu ya kuchimba dhahabu inatisha, idhibitiwe – 2
Wiki iliyopita makala haya yalihoji kwa nini hakuna anayeingia mgodini kupinga uchimbaji wa kasi kubwa bila udhibiti. Leo tunakuletea sehemu ya pili ya makala haya. Endelea…
Rais Karume, Maalim Seif ni Uamsho?
Kwa muda sasa nchi yetu imetikiswa. Imetikiswa si na kingine, bali ishara na viashiria vya udini. Tumepata misukosuko huko Buseresere kwa Wakristo kuamua kuchinja. Tumepata misukosuko huko Zanzibar kwa Padre Evarist Mushi kupigwa risasi na Kanisa kuchomwa moto.