JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Ukombozi wa taifa umeanzia Arumeru

Pole Sioi Sumary. Hongera Joshua Nassari. Nyota ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) inachanua. CCM waanze kujifunza kuwa kambi rasmi ya upinzani mwaka 2015.
[caption id="attachment_2" align="alignleft" width="158"]Deodatus BalileDeodatus Balile[/caption]
Haya ni maneno ya utangulizi niliyolazimika kuanza nayo katika safu hii ya Sitanii. Ikiwa mazingira hayatabadilika, nitakachokitabiri hapa ndicho kitakachotokea mwaka 2015.

Zambia inaihujumu Tanzania Tazara?

Sheria inatumika kuiua reli hiyo, wafanyakazi hoi
Mizigo tani 20,000 yarundikwa kwa mwaka mzima
Siku chache baada ya Serikali ya China kutangaza nia ya kuisadia Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) vifaa vitakavyoifufua reli hiyo, Chama cha Wafanyakazi TRAWU-TCPC kimesema njia pekee ya kuanza kuifufua reli hiyo ni kuondoa uongozi wa mameneja wote wa vitengo, na kuweka mameneja wapya wenye uwezo wa kufanya kazi kibiashara zaidi.

Messi wa Barcelona, Argentina ni kama Boko wa Azam na Tanzania

LICHA YA KUJITENGENEZEA REKODI NA KUTESA DUNIANI:

WIKI tatu zilizopita, mshambuliaji anayeaminika kuwa ndiye bora zaidi duniani hivi sasa, Lionel Messi, alivunja rekodi ya kuifungia mabao mengi zaidi timu yake ya Barcelona ya Hispania tangu ilipoundwa.

Waraka wa wanafunzi elimu ya juu nchini (1)

Ufuatao ni waraka wa wanafunzi wa elimu ya juu nchini kwa Serikali, kuhusu migomo na maandamano ya mara kwa mara hapa nchini. Umeandikwa na jopo la viongozi wa wanafunzi wa vyuo vikuu na wameupeleka serikalini. Wanatoa ushauri maridhawa wa namna ya kukomesha migomo kwa kuboresha sekta ya elimu, hasa kwa kuwapa fursa wanafunzi wote bila ubaguzi. Waraka huu ni mrefu na JAMHURI itauchapisha wote kuanzia leo. Endelea…

Kifo cha CCM ki wazi, suala ni lini kitatokea

Mengi yameandikwa juu ya ushindi wa Joshua Nassari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Jimbo la Arumeru Mashariki. Naomba wasomaji waniruhusu nami niweze kusema japo kwa ufupi mtazamo wangu juu ya ushindi wa kijana huyo.

Ubingwa mikononi mwa Simba, Yanga, Azam

*Boko naye asogelewa na ‘Kiatu cha Dhahabu’

Wakati Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ikiwa imeingia katika raundi ya 22, mwelekeo wa ubingwa hivi sasa umebaki mikononi mwa timu tatu za Simba, Azam na Yanga, zote za Dar es Salaam.