JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Juhudi za Lowassa kuihangaikia elimu zinapaswa kuungwa mkono

 

Naweza kumpenda au kumchukia sana Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, lakini hata iweje sitajizuia kumuunga mkono mtu yeyote akifanya jambo jema au lenye tija kwa taifa.

 

Siku chache zilizopita, Lowassa aliongoza harambee iliyokusanya Sh. milioni 530 kutoka kwa wadau wa maendeleo ya elimu – fedha ambazo Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho yeye mwenyewe ni mwanachama wake, kilichangia Sh. milioni 20.

 

Ije Jubilee nyingine ya malkia tushibe

Si mapumziko hata kidogo, maana ni sikukuu lakini waliofanya kazi wametoka na vinono. Wengi wataendelea kumwombea Mtukufu Malkia Elizabeth II adumu na serikali iendelee kuridhia maadhimisho ya sherehe zake.

Adui wa Waislamu ni utamaduni wa Kiarabu wa Ghuba

*Ukristo ama Uislamu na serikali si tatizo katu
Naomba nichangie hapa kama Mtanzania -na si kama Mwislamu au Mkristo au mpagani. Mosi, ni kweli kwamba kitabu cha yule padri Mzungu, Dkt. John Sivalon kinaleta shida sana mawazoni mwa watu. Lakini turejee kwenye ukweli wa kisomi, kwamba huwezi kuhitimisha jambo zito kwa kutumia chanzo kimoja.

Yah: Uzalendo uliondoka kama Ujamaa na Kujitegemea?

Wanangu, leo nimeamka nikiwa na siha njema kabisa na kufurahi kwamba sasa mmeanza kuyaona yale ambayo labda sisi watu tunaoonekana wazee, mnaweza kuyaangalia kwa kina na kuyatafutia ufumbuzi wa kina ili tuondoke hapa tulipo twende huko kulikokuwa kunatarajiwa na wengi.

Yai Sh. 900 hata mwendawazimu hakubali

Miongoni mwa mambo niliyoshindwa kuyaamini wakati wa vikao vya Kamati za Bunge vilivyofanyika Dar es Salaam wiki iliyopita, ni matumizi ya fedha za umma katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma kuhusu bei ya mayai.

Waziri Mukangara, Katibu Kamuhanda sema ukweli wote

Wiki iliyopita wahariri wa vyombo vyote vya habari nchini walikutana mjini Morogoro kujadili mustakabali wa tasnia ya habari nchini. Mkutano huo ulipaswa kufunguliwa rasmi na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara.  Waziri alikuwa na taarifa zaidi ya miezi miwili. Jumamosi ya wiki iliyopita ndipo akatuma ujumbe mfupi wa simu kwa Katibu Mkuu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Kajubi Mukajanga, akimweleza kuwa asingeweza kufika.