JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Brigedia Jenerali Aliasa Taifa

*Asema udini na ukabila ni ufa unaobomoa Taifa letu

 

Moja ya hotuba za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, zisizochujuka ni ile aliyoitoa pale Kilimanjaro Hotel mbele ya Klabu ya Waandishi wa Habari Tanzania Machi 13, 1995.

 

Katika mazungumzo yake siku ile alitaja nyufa tano zinazolitikisa  Taifa letu kuanzia kwenye paa, katika dari, kutani hadi kufikia katika msingi ule imara wa Taifa uliojengwa kwa muda mrefu. Nyufa zilizotajwa zilikuwa:-

 

* Muungano

* Kupuuza na kutojali

* Kuendesha mambo bila kujali sheria

* Rushwa, na

* Ukabila na udini.

 

Natabiri Nyalandu atakuwa tatizo

Siku chache baada ya uteuzi wa viongozi wakuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii – waziri na naibu wake, niliandika waraka mahsusi uliowahusu. Moja ya mambo niliyoyazungumza ni namna wizara hii ilivyo na vishawishi vingi vinavyotokana na ukwasi wake.

 

CCM iwabaini, iwatimue wanaoihujumu

Jumatano iliyopita, baadhi ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka kata mbili za Azimio wilayani Temeke na Tandale, Wilaya ya Kinondoni mkoani  Dar es Salaam, waliandamana ili kupinga hujuma walizodai zinavuruga uchaguzi mkuu wa ndani wa chama hicho na jumuiya zake zote unaoendelea hivi sasa.

Nidhamu itawapa wabunge heshima

WIKI hii tumeshuhudia michango mbalimbali ikitoka kwa wabunge kwenye ukumbi wa Bunge mjini Dodoma. Yametokea malumbano kati ya wabunge kadhaa na kiti cha Spika. Binafsi nilishuhudia tukio hili, hadi Mwenyekiti wa Bunge aliyekuwa amekalia kati cha Spika akaamuru mbunge mmoja kuondolewa ukumbini. Mabaunsa sita, walikwishajongea kwa nia ya kumtoa ukumbini, lakini yeye akajitoa mwenyewe.

 

Lundenga: Miss Tanzania imeitangaza nchi

Kwa muda wa miaka 18 iliyopita, mashindano ya Mrembo wa Tanzania yamekuza utamaduni, utalii na uwekezaji wa kigeni. Si hilo tu, mashindano haya yamewapa fursa mpya ya kujitambua wasichana Watanzania, anasema mwandaaji wa mashindano hayo, Hashim Lundenga.

 

Chadema sasa wadai rasmi Serikali ya Tanganyika

 

Hii ni sehemu ya maoni ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Tundu Lissu kuhusu Mpango wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) kwa mwaka wa fedha wa 2012/2013. Endelea

 

Katika maoni yetu kuhusu Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ilionyesha jinsi ambavyo “tafsiri hii mpya ya Makubaliano ya Muungano na Katiba ya Jamhuri ya Muungano imetiliwa nguvu kubwa na Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ambayo imeipa Zanzibar nafasi na ushawishi mkubwa katika utungaji wa Katiba Mpya.”