JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

January Makamba amefanya jambo la kuigwa

Mbunge wa Bumbuli mkoani Tanga, January Makamba, ametangaza kuwa amejipanga kuongeza kasi ya maendeleo ya elimu katika jimbo hilo, kazi itakayofanyika kwa kupitia Shirika la Maendeleo Bumbuli (BDC) kuanzia mwaka huu.

 

Programu hiyo itagharimu Sh. milioni 40 ikijumuisha vivutio kwa walimu na wanafunzi wa shule za sekondari; yote ikilenga kuongeza tija na umakini wa kujifunza na kusaidia juhudi zinazofanywa na serikali katika elimu.

Ardhi ya Tanzania inavyoporwa na matajiri matapeli

*Kambi ya Upinzani yaanika bungeni uozo wa kutisha

*Familia ya Chavda yavuna mabilioni na kutokomea

 

Hii ni sehemu ya hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Halima Mdee, aliyoitoa bungeni wiki iliyopita, akieleza namna ardhi ya Tanzania inavyohodhiwa na wafanyabiashara na matajiri matapeli…


MASHAMBA YALIYOBINAFSISHWA AMBAYO HAYAJAENDELEZWA

Mheshimiwa Spika, wakati akihitimisha bajeti ya ardhi mwaka jana, Waziri wa Ardhi aliliahidi Bunge lako Tukufu kwamba baada ya Bunge la bajeti wizara ingekwenda kufanya ukaguzi huru wa nani ametelekeza mashamba. Alisisitiza kwamba wawekezaji wote waliotelekeza mashamba “the honeymoon is over.”

Sinema kwa wasioona zaja

  Badala ya utaratibu wa zamani sasa waonyesha sinema wamebuni utaratibu mpya wenye kuwawezesha watu wasioona kuangalia sinema sambamba na watu wanaoona.   Teknolojia hii ya aina yake, iko sawa na zile zinazotumika kwenye ndege ikiwa angani, ambapo mtu anaweza…

Brigedia Jenerali aliasa Taifa (2)

Pamoja na malalamiko mengi na ya mara kwa mara, lakini ndugu zangu Watanzania wenzangu hawa wamejaaliwa uwezo mkubwa sana kiuchumi (have a very strong economic base). Hilo kamwe hawalitangazi wanaliacha kwenye “low profile”- mambo yao kimya kimya tu.

 

La Dk. Ulimboka linahitaji uchunguzi huru

Tumemaliza wiki mbili sasa tangu litokee tukio la kinyama la kumteka, kumpiga na kumuumiza vibaya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka. Tangu litokee tukio hili baya na la kinyama, mjadala umekuwa mkali na yameibuka maneno ninayoamini yanapaswa kupatiwa majibu na uchunguzi huru.

Weah: Mwanasoka aliyetamba dimbani, akatikisa katika siasa

Baada ya kumalizika kwa vita ya muda mrefu ya wenyewe kwa wenyewe huko Liberia, mwanasoka mstaafu, George Opong Weah, alitangaza kuwania urais wa nchi hiyo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, kisha akaanzisha chama kinachoitwa Congress for Democratic Change (CDC).