JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Danadana za Sheria ya Habari zitaisha lini?

Wiki iliyopita Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, amewasilisha bajeti ya wizara yake kwenye mkutano wa Bunge unaoendelea mjini Dodoma. Si nia yangu kujadili bajeti hii inayofikia wastani wa Sh bilioni 19. Na wala sitajadili danadana ilizopigwa bajeti hii, ambayo awali ilikuwa iwasilishwe Julai 18, lakini kwa mshangao ikasogezwa ghafla hadi Agosti 7, kisha kinyemela ikarejeshwa Julai 24.

Uzalendo: Mtihani wa kuwa raia

Huwa kila jamii yenye kujiheshimu hujiwekea vigezo vya watu wanaotakiwa kuwa ndani yake. Mataifa nayo – kwa kuwa yana mipaka yake yana watu ambao ruksa kuwa ndani – na wengine wote haruhusiwa kuingia, kukaa kwa muda mfupi au mrefu hadi kwa ruhusa maalumu (viza).

JKT ya wiki 3 kwa wabunge ni utani

Machi 17 mwakani imepangwa kuwa tarehe ya kurejesha upya mafunzo ya kijeshi katika Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), kwa mujibu wa sheria ambayo Serikali iliyafuta mwaka 1992.

Kilichonisikitisha ajali ya meli Zanzibar

Wiki iliyopita kwa mara nyingine taifa letu limeshuhudia majonzi ya aina yake baada ya Watanzania wengine wapatao 150 kupoteza maisha baada ya meli waliyokuwa wakisafiria kuzama.

Yanga, Simba ‘fowadi’ mbovu

Ikiwakilishwa na timu nne za Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club, Dar es Salaam Young Africans (Yanga), Azam FC zote za jijini na Mafunzo kutoka Zenji katika hatua za awali za michuano ya Kombe la Kagame, Tanzania ilipata fedheha kubwa katika mechi zilizochezwa siku ya kwanza na ya pili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mke wa Msekwa, wenzake wanavyotafuna nchi

*Kikao cha siku moja walipata Sh milioni 7

*Mjumbe mmoja asaini posho mara mbili

*Mkewe Mudhihir ambaye si mjumbe alipwa

 

Ufisadi unazidi kuwaandamana viongozi wa CCM. Safari hii, Mbunge wa Viti Maalumu, Anna Abdallah, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho pamoja na wajumbe wa Bodi hiyo, wanatuhumiwa kujilipa mamilioni ya shilingi. Ulaji huo umefichuliwa na Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Rose Kamili, katika hotuba yake ya makaridio ya mapato na matumizi ya mwaka wa fedha wa 2012/2013

 

BODI ZA MAZAO YA BIASHARA NA MAENDELEO YA KILIMO

Mheshimiwa Spika, kilimo cha mazao ya biashara hapa nchini kwa sasa kina changamoto nyingi. Changamoto hizo ni pamoja kukosa soko na bei za uhakika za mazao hayo.