JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Wazungu wanavyoitafuna Tanzania

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele ametoa taarifa kwa umma kuhusu udanganyifu unaofanywa na kampuni ya uchimbaji ndhahabu ya Aureus Limited ambayo zamani ilikuwa ikijulikana kama Minextech. Ifuatayo ni taarifa hiyo neno kwa neno…

 

Utangulizi

Kampuni ya Aureus Limited (zamani ilikuwa ikiitwa Mineral Extraction Technologies Ltd (Minextech) ni kampuni inayojishughulisha na uchenjuaji wa marudio ya dhahabu ya wachimbaji wadogo (gold tailings) kwa kutumia teknolojia ya kemikali ya sayanaidi (vat leaching).

Kikwete polisi wanaanza kuyeyusha heshima uliyojijengea

Mwaka 2008 nilibahatika kuwa mmoja wa watu waliopata fursa ya kusafiri na Rais Jakaya Kikwete kwenda jijini Washington, Marekani. Safari hii ilikuwa ikihusiana na mambo mbalimbali lakini kubwa ni kushawishi Serikali ya Marekani kuridhia Mpango wa Millennia Challenge Cooperation (Account) – MCC.

Kivumbi Ligi Kuu Bara chaanza

Michuano ya Ligi Kuu ya Soka ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu, inaanza kutimua vumbi kwenye viwanja saba tofauti, Jumamosi wiki hii. Agosti 31, mwaka huu, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), lilitoa ratiba inayoonesha kuwa bingwa wa ligi hiyo atapatikana Mei 18, mwakani, wakati timu zote 14 zinazoshiriki zitakapokuwa uwanjani kuhitimisha mechi zake 26 kila moja.

Tanzania siku si nyingi haitatawalika

Kwa siku za karibuni nchi yetu imegubikwa na mambo mengi ya kuudhi. Taifa linapokuwa na polisi wezi, waporaji na wauaji, usitarajie kwamba litaendelea kuwa salama. Taifa linapokuwa na majaji kama wale tulioambiwa na Mheshimiwa Tundu Lissu, hakika tumekwisha.

Mwakyembe, Chambo wasitishwe

BAADHI ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), wamemwandikia barua Katibu Mkuu Kiongozi, Ikulu, Balozi Ombeni Sefue wakidai kuwa Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe anafanya kazi kwa kutumia majungu anayopelekewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Omar Chambo.

Yah: Nguvu ya maji yaja, mtaua wangapi?

Wanangu, ka-jua ka leo kananikumbusha mandhari ya miaka mingi kabla Tanganyika haijaanza kuwa jangwa la kutisha na kushindwa kuhimili hali ya ukame na wakati mwingine kukosa maji ambayo yanasababisha hadi tukose umeme na kusababisha kuyumba kwa uchumi  wa mtu mmoja mmoja na nchi.