JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Simba wanataka Kaseja adake, awafungie mabao?

Wakati mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ulimalizika Jumapili iliyopita, kipa namba moja wa klabu ya Simba na timu ya taifa (Taifa Stars), Juma Kaseja, amehitimisha ngwe hiyo kwa huzuni, mashaka na wasiwasi mkubwa kutokana na kutukanwa, lawama na vurugu alizofanyiwa kuanzia Morogoro hadi jijini Dar es Salaam.

Ligi Kuu Bara ‘yaanza upya’

Ushindi wa Dar es Salaam Young Africans (Yanga) wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Mgambo katika mashindano ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Jumatano iliyopita, na sare ya bao 1-1 kati ya mabingwa watetezi, Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club ya jiji na Polisi Morogoro siku hiyo, ulizifanya Yanga na Simba kufikisha pointi 23 kila mmoja. Hali ya kulingana pointi ya mahasimu hao wakuu wa soka nchini imeibua msisimko mpya kwa mashabiki wa pande zote.

Ndugu zangu, nchi inateketezwa

Wapendwa, nimeshindwa kujua simanzi hii iliyonipata niielekeze kwa nani. Kilio hiki nakileta kwenu ili kwa pamoja tuweze kupata jibu la hiki kinachojaribu kukieleza hapa.Wiki iliyopita nilisafiri kutoka Dar es Salaam hadi Kyela mkoani Mbeya kwa kutumia gari. Nilirejea Dar es Salaam kwa usafiri huo huo. Njiani nilishuhudia mambo kadhaa ambayo naomba sana ndugu zangu tushirikiane kuyajadili.

Waingereza wanapoanza kufukua makaburi

*Walionyanyaswa na Savile walikuwa wapi akiwa hai?

Mwaka uliopita nilikuwa miongoni mwa maelfu ya watu waliokuwa mitaa ya Roundhay, Leeds, baada ya kifo cha Jimmy Savile.

Kenya, Uganda, Rwanda wanatuacha solemba

Kwa zaidi ya wiki sasa nipo hapa Nairobi, Kenya, nikihudhuria mafunzo ya uandishi wa habari za masuala ya kifedha, hasa bajeti ya Serikali. Mafunzo haya ni ya muda wa wiki mbili. Katika mafunzo haya tunapewa mifano kutoka sehemu mbalimbali na wakubwa kutoka Serikali ya Kenya wanawasilisha mada.

Dk. Nagu alichomfanyia Sumaye

Barua hii imeandikwa na watu waliojitambulisha kuwa ni wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao ni Wajumbe wa Mkutano Mkuu Wilaya ya Hanang’. Iliandikwa Oktoba 19, mwaka huu na kupelekwa kwa Katibu Mkuu wa CCM-Taifa. Kimsingi inapinga ushindi wa nafasi ya NEC wa Dk. Mary Nagu dhidi ya Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye.

YAH: KUPINGA MATOKEO YA UCHAGUZI NAFASI YA MJUMBE WA HALMASHAURI KUU TAIFA (NEC) WILAYA YA HANANG’

Mheshimiwa Katibu Mkuu, kichwa cha habari hapo juu chahusika. Sisi wenye majina na saini zetu hapo chini kwenye kiambatanisho cha barua hii ni viongozi na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM (W) ya Hanang’.