JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Kituo cha Mabasi Ubungo: Mgodi wa mafisadi

*Hoja ya Mnyika yawekwa kapuni

Utangulizi

Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT) kilifunguliwa rasmi Desemba 6, 1999 pamoja na mambo mengine, uanzishwaji wa kituo hiki ulikuwa na madhumuni ya kutoa huduma kwa wasafiri pamoja na watumiaji wengine na pia kuongeza mapato ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Kikwete alivyowalilia Sharo Milionea, Mlopelo, Maganga

Rais Jakaya Kikwete, ameelezea kustushwa na kusikitishwa na vifo vya wasanii maarufu nchini, Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’, Khalid Mohamed ‘Mlopelo’ na John Stephano Maganga.

Yanga inavyoipiku Simba

Hatua ya uongozi wa Yanga kuingia mkataba na kampuni ya kimataifa ya ujenzi inayojulikana kama Beijing Constructions ya China, imezidi kuwapiku mahasimu wake wakubwa wa soka nchini, Simba, kutokana na kuendelea kuwazidi kete ya mafanikio ndani na nje ya uwanja.

Tumezubaa ardhi ya Tanzania inakwisha!

Mwaka 1958, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alizungumza maneno ya maana sana kuhusu ardhi.

 

Alisema, “Katika nchi kama yetu, ambayo Waafrika ni maskini na wageni ni matajiri, kuna uwezekano mkubwa kwamba Mwafrika akiruhusiwa kuiuza ardhi, katika miaka themanini au miaka mia ijayo, ardhi yote ya Tanganyika itamilikiwa na matajiri wageni, na wenyeji watakuwa watwana. Lakini hata kama wageni wasingekuwa matajiri, litaibuka tabaka la Watanganyika matajiri wajanja. Tukiruhusu ardhi iuzwe kama kanzu, katika muda mchache, kutakuwa na kundi dogo la Waafrika wakiwa na ardhi na walio wengi watakuwa watwana.”

Asanteni Watanzania, tumethubutu, tuungeni mkono

Wiki hii Kampuni ya Jamhuri Media Limited inaandika historia ya kipekee. Juni 28, 2011 kwa ushirikiano wa waandishi wa habari wanne, tulisajili kampuni ya Jamhuri Media Limited. Oktoba 5, 2011 tulipata usajili wa Gazeti Jamhuri. Desemba 6, tukachapisha nakala ya kwanza ya Gazeti Jamhuri. Ni wazi basi, kuwa wiki hii tunahitimisha mwaka mmoja na nusu wa kampuni kusajiliwa, lakini pia tunatimiza mwaka mmoja wa kuendesha Gazeti Jamhuri.

Waliotoa rushwa waajiriwe polisi wanaugua ujinga

Tanzania inaelekea kuwa nchi ya watu walalamishi, wanaolia siku zote kulalamikia matatizo mbalimbali vikiwamo vitendo vya rushwa, ingawa wengi wao ni vinara wa kushawishi kutoa na kupokea rushwa. Cha kushangaza ni kwamba watoa rushwa ndio mara nyingi wamekuwa watu wa kwanza kulalamikia na kulaani uovu huo baada ya ‘kulizwa’ na wapokea rushwa katika mazingira mbalimbali.