JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Uhuru umeyeyusha matarajio yetu

Desemba 9, mwaka huu, Watanzania tumeadhimisha miaka 51 ya Uhuru wa nchi yetu, huku wengi wetu wakikabiliwa na maisha magumu kupindukia. Binafsi ninaamini kuwa ni unafiki kusema Tanzania haina cha kujivunia, lakini pia ni unafiki kusema Serikali kupitia Uhuru huu, imeboresha maisha ya wananchi.

Mihadarati sasa yapigiwa upatu

Nilipokuwa nchini Ghana kwa mafunzo ya vitendo mwishoni mwa miaka ya ’80, nilishangazwa na daktari mmoja. Nakumbuka ilikuwa katika Korle-Bu Teaching Hospital ya Chuo Kikuu cha Accra, na bado sijausahau mtaa wake – Guggisberg Avenue katika mji mkuu, Accra.

Yah: Kama ningekuwa Waziri wa Usalama Barabarani

Wanangu, nawapa kongole ya kutimiza miaka 51 ya Uhuru mlionao hivi leo, nawapongeza kwa kuwa sisi wana-TANU ni kama ndoto ya kuamini kuwa tumeweza kuhimili vishindo vya wakoloni kwa kipindi chote hiki.

Sarafu moja Afrika Mashariki ni mtego

Wiki iliyopita hapa nchini umekuwapo mjadala wa kiuchumi, unaohoji mpango wa kuharakisha matumizi ya sarafu moja katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mjadala huu umehusisha wadau mbalimbali, akiwamo Balozi wa Tanzania nchini Ubeligji, Dk. Diodorus Kamala.

DC Geita ageuka kituko

Mkuu wa Wilaya (DC) ya Geita, Manzie Mangochie, ameingia kwenye vita ya maneno na waandishi wa habari wilayani humo. Katika hatua ambayo haijapata kutekelezwa na DC yeyote, sasa Mangochie, anataka taarifa za waandishi wote, pamoja na sifa zao za elimu. Hoja yake ni kwamba anataka kuandaa “Press Cards”; jambo ambalo kwa miaka yote limekuwa likifanywa na Idara ya Habari (Maelezo).

Mwenyekiti Musukuma apuuzwe

Magazeti kadhaa yameripoti kwamba Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Joseph Musukuma, amewaambia wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji cha Nyawilimilwa kilichopo Kata ya Kagu, kwamba hatakuwa tayari kupeleka maendeleo katika kata hiyo kwa sababu inaongozwa na Diwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).