JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Taifa Stars rarua Ethiopia

Januari 11, mwaka huu, mashabiki wa soka na Watanzania kwa jumla wataelekeza macho na masikio yao mjini Adis Abab, Ethiopia, wakati Taifa Stars itakapojipima nguvu na wenyeji wao.

Kikwete chukua hatua nchi inameguka vipande

Wiki iliyopita yametokea maandamano mjini Mtwara. Maandamano haya kwa yeyote anayeyaangalia kwa jicho la kawaida yalikuwa na nia njema. Yalilenga kuwapa fursa Watanzania wenyeji wa Mkoa wa Mtwara, kueleza malalamiko yao na haja yao ya kupata faida ya gesi. Wanataka badala ya gesi kusafirishwa kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam bomba lisijengwe.

Kuna umuhimu wa wafanyabiashara ‘kunolewa bongo’

Hongera sana ndugu wasomaji wa JAMHURI kwa kuuanza Mwaka Mpya wa 2013. Wiki kadhaa huko nyuma tulichapisha makala katika safu hii iliyokuwa na makosa katika kichwa cha habari, hivyo kuleta usumbufu wa kimantiki kwenu wasomaji.

Kichwa hicho kilichokosewa kilisomeka hivi: “Wafanyabiashara wanapaswa “kuolewa bongo zao”. Tunapoanza Mwaka Mpya nimeona ni busara niirudie makala ile katika maana na dhana niliyoikusudia.

Mrina Annex: Kivuli cha wakware Arusha

Si mara yangu ya kwanza kufika Arusha, lakini hii ni safari yangu ya kwanza kuzuru Arusha ikiwa “imepachikwa” hadhi ya kuitwa jiji. Kwangu mimi, Arusha ni “zizi.” Kama wingi wa watu ndiyo kigezo pekee cha mji kupandishwa hadhi na kuitwa jiji, basi watawala wetu watakuwa wanakosea.

Yah: Kama ningekuwa waziri wa dawa na matibabu…

Wanangu, poleni na kazi na hongera sana kwa kuvuka mwaka 2012. Nasikia mnapeana “Happy New Year” kila ninakopita na mnashangilia kwa nguvu, sina hakika mnashangilia kwa sababu zipi, lakini nafikiri kuumaliza mwaka siku hizi ni kazi ya ziada kutokana na maradhi na misukosuko mingi ya maisha.

Mwaka 2013 uboreshe michezo Tanzania

Tangu mwaka 1974 wakati Filbert Bayi alipoweka rekodi mpya ya mita 1,500 duniani, Tanzania haijapata mafanikio mengine makubwa kiasi hicho katika riadha na hata michezo mingineyo.