JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

FASIHI FASAHA

Tunakubali rushwa ni adui wa haki?

“Rushwa ni adui wa haki; sitapokea wala kutoa rushwa.”

Nimeanza na kauli hiyo kwa dhamira ya kukumbuka na kuuliza, “Wazalendo wa Tanzania wameikubali, wameizingatia na wanaitekeleza?”

FIKRA YA HEKIMA

Wanafunzi IFM nao wachunguzwe

Kero za uvamizi, uporaji mali, ubakaji na ulawiti dhidi ya wanafunzi wa Taasisi ya Usimamizi wa Fedha (IFM), zitapatiwa ufumbuzi wa kudumu ikiwa uchunguzi unaofanywa na Jeshi la Polisi utawalenga pia wanafunzi hao.

Muungano ndiyo mboni ya Tanzania (7)

Watu mnaweza kubishana kwa hoja, lakini si kwa kukamiana nani ni nani Visiwani Zanzibar. Kila mtu anataka, na ni haki yake kila mwananchi kutambuliwa kama yupo. Kutambuliwa huko kunafikiwaje? Vyama vyote vya upinzani vina lengo kuu moja tu- kuingia serikalini na kuboresha maisha ya wananchi kiuchumi, kielimu, kiafya na kiutawala bora. Njia zipi zitumike kuyafikia malengo hayo? Ndiyo ngoma inayochezwa kwenye uchaguzi huru.

IGP Mwema heshima uliyoijenga inapotea

Miezi ya Desemba 2012 na Januari, 2013 imenitia hofu. Imenitia hofu baada ya kuwapo matukio mengi ya wizi, ujambazi na ukatiri dhidi ya binadamu. Wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha wamelazimia kuandamana baada ya majambazi kuwa wanawavamia kwenye mabweni yao na kuwapora kompyuta za mkononi, fedha na vitu vya thamani. Imeelezwa kuwa hadi wanafikia uamuzi huo tayari walikwishaporwa laptop zipatazo 300.

Kashfa mpya Red Cross

*Dk. Nangale ‘achukua’ mitambo ya redio

Redio ya Sibuka imeingia katika kashfa nzito baada ya kubainika kuwa mitambo inayotumia redio hiyo kurusha mawimbi ya sauti ni mali Chama cha Msalaba Mwekundu (TCRS).

RATIBA YA LIGI KUU YA UINGEREZA

Jumamosi 19 Januari 2013: 12:00 – Chelsea v Arsenal Stamford Bridge 12:00 – Liverpool v Norwich Anfield 12:00 – Man City v Fulham Etihad Stadium 12:00 – Newcastle v Reading Sports Direct Arena 12:00 – Southampton v Everton St. Mary’s…