JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

FIKRA YA HEKIMA

 

2015 tuwakatae wabunge, mawaziri wa aina hii

Kwa hakika Watanzania hatuna sababu ya kuwarejesha madarakani wanasiasa hawa, kwa vile wametudhihirishia wazi kuwa nia yao ilikuwa ni zaidi ya kutuongoza na kututumikia.

Ninazungumzia wabunge na mawaziri wasiopokea simu za wananchi wa kawaida. Waswahili wanasema kufanya kosa si kosa; kurudia kosa ndiyo kosa.

Waishio mabondeni wahame; wahamie wapi?

Umekuwa wimbo wa kila ufikapo msimu wa mvua za masika, kuwasikia viongozi wa Serikali wakihimiza kwamba waishio mabondeni wahame, kwa vile wanaishi kwenye mazingira hatarishi ya maisha yao na mali zao.

China: Mkombozi pekee uchumi wa Afrika

Historia inazungumza mambo mazuri juu ya Afrika. Inaitaja Afrika kama chimbuko la maendeleo. Binadamu wa kwanza duniani anatajwa kuishi Afrika. Olduvai Gorge iliyopo Arusha nchini Tanzania, inatajwa kama eneo alikoishi binadamu wa kale zaidi ya miaka milioni mbili iliyopita.

NHC: Hatuhusiki ujenzi ghorofa lililoanguka

Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limejitokeza na kukana kuhusika na ujenzi wa jengo la ghorofa 16 katika Mtaa wa Indira Gandhi, jijini Dar es Salaam, ambalo lilianguka wiki iliyopita.

Mifugo yaharibu Pori la Akiba Maswa

*Wanasiasa, wafanyabiashara washushiwa lawama

Maelfu ya ng’ombe na mifugo mingine imeingizwa ndani ya Pori la Akiba la Maswa.

Inakadiriwa kuwa asilimia 30 hadi 40 ya pori hilo imemezwa na mifugo hiyo. Wingi wake umesababisha wanyamapori wengi wakimbie.

Mjue Bestizzo wa sasa

*Alianza kwa Muumin, kisha Dimond

*Sasa amedakwa na Wema SepetuNi msanii chipukizi, kijana mdogo mwenye umri wa miaka 21. Kwa sasa amedakwa na msanii maarufu na Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu. Huyu kijana si mwingine yeyote bali ni Best Werema maarufu kwa jina la Bestizzo. Kwa sasa ni mwajiriwa katika kampuni ya Wema Sepetu inayojulikana kama Endless Fame Production.