JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Tumeacha kuheshimu sheria, tumekwisha

Wiki hii nimekuwa hapa jijini Johannesburg. Nimekuja hapa Afrika Kusini kwa nia ya kumuona Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda, aliyetekwa, akapigwa, akaumizwa, akatobolewa jicho, akang’olewa meno na kucha. Ametiwa ulemavu wa kudumu. Ni masikitiko makubwa.

Mradi wa WB hatarini

*Ni kisima cha maji kilichogharimu Sh mil 50

*Tajiri anataka apewe Sh mil 22 kukinusuru

Wakati Watanzania wengi wakikosa maji safi na salama, mradi wa kisima cha maji eneo la Mpeta katika Manispaa ya Temeke, Dar es Salaam, uliofadhiliwa na Benki ya Dunia (WB), uko hatarini kutoweka.

TFF, Simba, Yanga wanaua uwekezaji soka la vijana

Karibu kila mdau wa michezo ninayezungumza naye kuhusu mustakabali wa maendeleo ya tasnia hiyo hapa Tanzania, anagusa uwekezaji kwa vijana. Nilivutwa na kuamini katika uwekezaji wa soka la vijana, baada ya serikali kumwajiri kocha wa timu ya Taifa, kutoka Brazil, Marcio Maximo.

FASIHI FASAHA

Watanzania tunakinyanyasa, kukibeua Kiswahili – 2

 

Juma lililopita nilizungumzia lugha yetu ya Kiswahili. Katika makala yale tuliona baadhi ya maandishi yenye kauli zinazoonesha mashaka au wasiwasi wa kunyanyaswa na kubeuliwa Kiswahili.

Haya nayo yana mwisho

Ninapotafakari mwenendo wa kiti cha Spika, sioni kama kuna umuhimu wa kuwa na Bunge.

Kumbe basi, Tanzania tunaweza kuendesha mambo bila kuwa na hiki chombo ambacho katika nchi nyingine, ni chombo kitakatifu.

FIKRA YA HEKIMA

Serikali inapodhamiria kukandamiza wanyonge

 

Kuwapandishia nauli watu wanaoshinda na kulala na njaa ni sawa na kuwachimbia kaburi; maana sasa watashindwa kwenda kujitafutia riziki ya kujikimu na familia zao, na hatimaye watakufa kwa kukosa chakula.