JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Bila ardhi masikini hawa watakwenda wapi?

Kabla ya kuendelea, niwapongeze viongozi wote wakuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Nampongeza mno Waziri Anna Tibaijuka, na Katibu Mkuu Patrick Rutabanzibwa (PR).

Yah: Tuliangalie sakata la elimu kwa sasa [2]

Wiki jana nilizungumzia juu ya elimu ya kambo wakati nikihitimisha barua yangu. Nilijaribu kuangalia tofauti za elimu ya sasa na ya zamani japokuwa hazipaswi kufananishwa kutokana na mitaala na manufaa baada ya masomo. Sisi tulifundishwa kujitambua na kujitegemea na ninyi kwa sasa mnafundishwa kutegemea na kutojitambua.

FASIHI FASAHA

Watanzania tunakinyanyasa,

tunakibeua Kiswahili – 7

Sina budi kutoa shukrani kwa wale wote walioniunga mkono katika mada hii ya Watanzania tunakinyanyasa na kukibeua Kiswahili. Ni dhahiri Watanzania wanatambua na wanajali lugha yao ya Kiswahili. Asante. Baadhi ya Waswahili wanasema kuwa lugha ya kaya, kabila, rika, masikani na vijiweni, na hata sehemu zetu za kazi, au michezo zisiwe ni vigezo kuwa Watanzania hawakithamini Kiswahili. Hizo ni lugha za msimu tu.

 

FIKRA YA HEKIMA

Wawekezaji wazawa waungwe mkono

Watanzania tumejenga kasumba mbaya ya kuwathamini wawekezaji wa kigeni. Wakati huo huo tumekuwa kikwazo kwa wawekezaji wazawa!

Kashfa zimelilemea Jeshi la Polisi

Wakati fulani wabunge waligombana na aliyekuwa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Omar Mahita. Hoja ilikuwa kwamba Jeshi la Polisi lilistahili kuvunjwa ili liundwe upya. Wakatoa mfano wa Jeshi la kikoloni la King African Rifles (KAR), lilivyovunjwa baada ya maasi ya mwaka 1964 na kuundwa kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Stars tupeni raha Watanzania

Timu ya Soka ya Taifa (Taifa Stars) inatarajiwa kushuka dimbani Juni 8 mwaka huu, kucheza na Morocco katika mchezo wa kuwania kufuzu kushiriki Mashindano ya Kombe la Dunia 2014 yatakayopigwa nchini Brazil.