JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Vionjo vya marais wa Marekani

*Barack Obama: Mweusi wa kwanza kuiongoza

* Kennedy: Ndiye Mkatoliki pekee kukubalika

*Franklin: Alidumu muda mrefu madarakani

*William Henry: Aliongoza kwa siku 32 pekee

Kwa mujibu wa Katiba ya Marekani, Rais wa Marekani ndiye mkuu wa nchi na Serikali ya Marekani. Ndiye mkuu wa Serikali ya Shirikisho, na ofisi ya rais ndiyo kubwa kiutawala nchini humo. Rais pia ndiye Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Marekani.

Marekani ni fursa, Watanzania tuikumbatie

Taifa la Marekani limefika mahala sasa linaliamini taifa la Tanzania. Miaka ya 1960 na 1970 kutokana na Vita Baridi kati ya Marekani na Urusi, ilikuwa vigumu kwa Marekani kufanya kazi na Tanzania.

Marekani inavyoinufaisha Tanzania kupitia AGOA

Rais wa Marekani Barack Obama yupo hapa nchini kwa ziara ya kiserikali. Ujio wa Obama umekuwa na shamrashamra nyingi si tu Dar es Salaam bali macho na masikio ya Watanzania wote yameelekezwa katika safari hii. Ni ziara ambayo pamoja na mambo mengine mengi, pia imekusudia kuimarisha uhusiano baina ya Tanzania na Maekani.

MCC, yang’arisha miradi ya kijamii Tanzania

. Umeme wapewa kipaumbele

Mradi mkubwa wa ukarabati na upanuzi wa mfumo wa kusambaza umeme utakaohusisha mikoa 10, wilaya 24 na vijiji 356 Tanzania umezinduliwa hivi karibuni, ikiwa ni matunda ya Mfuko wa Changamoto za Milenia (MCC).

Familia ya Barack Obama ni wanamichezo mahiri

Rais wa Marekani, Barack Obama, mke wake, Michelle, watoto wao, Malia na Natasha (Sasha) ni familia ya wanamichezo mahiri.

Barack Hussein Obama ni nani?

 

Barack Hussein Obama alizaliwa Agosti 4, 1961. Ni Rais wa 44 na Rais wa sasa wa Marekani. Ni Raia wa Marekani na Rais wa kwanza mwenye asili ya Afrika kushika wadhifa huo. Pia ni mtu wa kwanza aliyezaliwa Hawaii kushika nafasi hiyo.