JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Nami naomba niushutumu Usalama wa Taifa

 

Desemba 6, 2011 kwenye toleo la kwanza la Gazeti JAMHURI, tuliweka bayana msimamo wetu juu ya masuala yanayolihusu Taifa letu.

MISITU & MAZINGIRA

Uharibifu misitu: Janga linaloiangamiza Tanzania (1)

Tanzania ilibahatika kuwa na hazina kubwa ya misitu ya asili karibu katika kila wilaya na mkoa. Takwimu za mwaka 1998 zinaonesha kuwa Tanzania Bara ilikuwa na hekta (ha) milioni 13 za misitu iliyohifadhiwa kisheria (ikiwa ni zaidi ya misitu 600 ya Serikali Kuu na misitu 200 ikimilikiwa na Serikali za Mitaa, yaani, Halmashauri za Wilaya.

FASIHI FASAHA

Watanzania tunakinyanyasa, kukibeua Kiswahili – 4

“Hali yetu ya Kiswahili hivi sasa si nzuri. Kuna makosa mengi katika matumizi. Inaelekea ufundishwaji wa Kiswahili ni tatizo. Vipi Kiswahili kiwe tatizo wakati ni lugha ya msingi na Taifa? Taifa halijatoa umuhimu wa lugha ya Kiswahili, kifundishwe kuanzia shule za msingi hadi chuo kikuu. Lakini Kiswahili gani kifundishwe? Hata wanaojua Kiswahili wanakiharibu.”

RC Arusha anaendekeza ujinga dhidi ya Lema

Miaka miwili iliyopita Rais Jakaya Kikwete alipofanya uteuzi wa wakuu wa mikoa, nilifurahi. Nilifurahi baada ya kusikia wamo vijana walioteuliwa, na hasa mmoja tuliyekuwa tukifanya kazi wote chumba cha habari Majira, Fatma Mwassa. Huyu sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora na anaendelea vyema.

Mchezo wa vinyoya unaweza kuibeba Tanzania Olympics

Hatimaye wadau wamejitolea kuufufua mchezo wa vinyoya, uliopoteza hadhi yake licha ya kuitangaza Tanzania kimataifa miaka ya 1960 na 1970.

Yah: Laiti lingepigwa baragumu wafu wafufuke

 

 

 

Kuna wakati huwa naona kama ndoto ninapowakumbuka baadhi ya watu. Namkumbuka sana marehemu baba yangu, kwa mtazamo wake na uamuzi wa kifamilia kwa wakati ule. Naona jinsi alivyokuwa na mtazamo wa kitaifa zaidi na si kifamilia.