Category: MCHANGANYIKO
Wakimbia makazi kukwepa operesheni okoa
Siku chache baada ya maofisa wanaoendesha Operesheni Okoa Mazingira iliyofanyika katika Kijiji cha Usinge wilayani Kaliua, kutuhumiwa kumuua, Kipara Issa (39), kwa tuhuma za kumiliki silaha kinyume na sheria, baadhi ya wanaume katika kijiji hicho wamelazimika kuzikimbia familia zao kwa hofu ya kukamatwa na maofisa hao.
Yah: Utitiri wa vyombo vya habari na habari inayotolewa
Kuna wakati nakumbuka miaka yetu ya giza totoro la habari, kwamba habari ilikuwa ni kitu nyeti ambacho mwananchi alipaswa kujua kwa gharama ya muda au kwenda safari kuitafuta, leo habari unaipata mahala ulipo na unachagua unataka habari gani.
Michael Jackson anaongoza kwa utajiri
Mfalme wa muziki wa aina ya Pop, Marehemu Michael Jackson, ametajwa kuwa kati watu maarufu duniani waliofariki dunia ambao kazi zao zimeingiza kiasi kikubwa cha fedha katika kipindi cha mwaka mmoja, kuanzia Oktoba 2012 hadi Oktoba 2013.
Hammer Q auponda muziki wa Bongo Fleva
Mwimbaji Nyota wa Muziki wa Taarab nchini, Hussein Mohammed ‘Hammer Q’ (pichani kushoto) amesema kuwa alifanya muziki wa bongo fleva kama njia ya kutafuta njia ya kufanikiwa katika tasnia ya muziki.
Brandts aliisubiri Simba kuwapumzisha wakongwe?
Kati ya mambo yaliyojadiliwa na wapenzi wa soka wiki iliyopita, ni pamoja na matokeo ya mechi ya watani wa jadi — Wekundu wa Msimbazi Simba Sports Club (Mnyama) ya jijini na Dar es Salaam Young Africans (Yanga) yenye makao yake mitaa ya Jangwani na Twiga, baada ya timu hizo kutoka sare ya mabao 3-3 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliopigwa katika Dimba la Taifa Dar es Salaam.
Ubaguzi wa rangi washika kasi Ulaya
Kuna kila hali inayoonesha kuwa kwa sasa vitendo vya ubaguzi wa rangi, vinazidi kushika kasi katika soka barani Ulaya, pamoja na kuwa kumekuwa na kampeni za hapa na pale za kupiga vita dhidi ya vitendo vya ubaguzi.