JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Vibwanga vya Waziri Lazaro Nyalandu

*Madudu yake yanamchafua Rais Kikwete

Mara tu baada ya mawaziri wanne kujiuzulu na wengine kuondolewa kutokana na tuhuma za ukiukwaji wa haki za binadamu katika Operesheni Tokomeza, mwandishi mmoja aliandika makala iliyokuwa inasomeka, “Kikwete ana mkosi gani na mawaziri wake?”

Vituko vya DC Geita

Na Victor Bariety, Geita

Sehemu ya kwanza ya makala hii ilielezea vituko vinavyofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Geita, Omari Manzie Mangochie, vikiwamo vya kuzuia ujenzi wa mnara wa simu za mkononi na kutangaza vita na waandishi wa habari. Sasa endelea na sehemu hii ya pili.

Mkuu wa Wilaya ya Geita, Omari Manzie Mangochie ambaye anatajwa kama kiongozi anayezalisha migogoro na kukwamisha shughuli za maendeleo wilayani hapa. Anatuhumiwa pia kumng’oa Mwenyekiti wa Chama chake cha Mapinduzi (CCM) wa kijiji cha Mnyara, hivyo kuwapatia wapinzani mwanya wa uongozi.

Katika tuki hilo la aina yake, Mangochie baada ya kumvua uongozi Mwenyekiti wa Kijiji cha Mnyara, Makoye Roboyanke, aliitisha uchaguzi mdogo na kuwaamuru wananchi kupiga kula za wazi mgongoni mwa wagombea kinyume cha taratibu za uchaguzi.

Kitendo hicho kilizua tafrani kubwa kwani pamoja na wananchi kukubali matakwa ya Mkuu huyo wa wilaya kwa kuwachagua viongozi wao nyuma ya migongo, CCM kilichokuwa kimeweka mizizi eneo hilo kilibwagwa na kusababisha msimamizi wa uchaguzi kukimbia na matokeo ili kujinusuru na kipigo kutoka kwa wananchi hao.

Inadaiwa kuwa uamuzi huo wa Mangochie wa kumvua uongozi kada huyo wa CCM bila kufuata utaratibu umesababisha wananchi wa eneo hilo kukihama chama hicho tawala na kujiunga na vyama vya upinzani ambavyo hapo awali havikuwa na nguvu kwenye kijiji hicho ambapo wameiomba Serikali kuingilia kati mgogoro huo.

Akizungumza na JAMHURI kijijini hapo hivi karibuni, mwenyekiti huyo wa kijiji alisema uamuzi huo wa Mangochie umemdhalilisha na umeonesha ni jinsi gani asivyoheshimu vikao halali vya CCM.

KAGAME NI MTIHANI Viongozi Maziwa Makuu waufanye kwa Uangalifu

Ni wazi kwamba nafasi inayoshikiliwa na Uganda na Rwanda katika roho ya uchumi wa Marekani na Uingereza ni kubwa kuliko nchi yoyote ile katika eneo la Maziwa Makuu kwa sasa.

Hakika Marekani na Uingereza wamelipa gharama kubwa kutengeneza miundo ya kiserikali, nguvu za kijeshi na saikolojia za kisiasa zinazoongoza nchi hizo miaka ya karibuni.

Watu walijiuliza maswali mengi kunako miaka ya tisini juu ya nguvu za Museveni na baadaye kasi ya RPF kuitwaa Rwanda, nchi ambayo ilikuwa imeanza kuimarika kama zilivyokuwa nchi nyingine barani Afrika. Hasa nchi ambazo zilikuwa zimeishi kwa amani toka uhuru mpaka miaka hiyo.

Mwanzoni mwa miaka ya tisini Rwanda ilikuwa na fedha yenye thamani kubwa. Ilikuwa pia na msaada mkubwa wa kijeshi kutoka Ufaransa. Raia wake walikuwa na kipato kizuri cha kutosha. Ilikuwa thabiti.

Matatizo yaliyokuwapo Rwanda miaka ya tisini yaliakisi matatizo yaliyokuwapo kwingineko barani Afrika kama vile vita za wenyewe kwa wenyewe, uongozi mbovu na uamuzi usiyo na tija, ufisadi wa wachache, upendeleo wa kikabila (Wahutu), undugu (nepotism) na zaidi suala la wakimbizi.

Wakimbizi wa Rwanda miaka ya ‘tisini mwanzoni’ walikuwa ni Watutsi waliokuwa wameikimbia nchi baada ya mapinduzi mwaka 1959 yaliyoiondoa dola ya mfalume Kigeri V muda mfupi kabla ya uhuru. Rwanda haikutofautiana na nchi nyingine nyingi barani Afrika.

Ukiilinganisha Rwanda ya sasa ya Kagame ambayo wapinzani wake wanaviziwa na kuuawa hata wakiwa nje ya nchi! Rwanda ambayo wakati wa uchaguzi raia wanapotea kimya kimya na baadhi kuokotwa wakiwa mizoga!

Kipande, Magesa wakoroga ICT bandari

 

Madeni KipandeMamlaka ya Bandari Tanzania imegeuzwa sehemu ya ulaji wa hali ya juu. Hata hivyo, kutokana na mtandao mpana wa kuchota fedha unaoanzia wizarani hadi bandarini, yeyote anayetaka kuonesha paka yuko wapi, basi anaishia ama kufukuzwa kazi kwa njia ya vitisho, au kufanyiwa ‘kitu mbaya’.

Mkurugenzi Mkuu, Madeni Kipande, anamkingia kifua Mkurugenzi wa ICT, Phares Magesa, ambao kwa pamoja wanatuhumiwa kuzamisha jahazi la bandari Tanzania.

Baada ya kuchapisha sehemu ya kwanza ya matukio yanayoendelea bandarini, wiki hii JAMHURI inakumegea sehemu tu kati ya madudu mengi yanayoendelea bandarini, ambayo kwa kila hali yanadhihirisha kuwa Mkurugenzi Mkuu, Madeni Kipande, ama hajui kitu kinachoitwa utawala wa sheria, au amedanganywa na watu wanaombeba pale Ikulu, hivyo amepoteza mwelekeo.

Ifuatayo ni sehemu ya barua ya ushauri wa kitaalamu, ambayo ilitolewa na aliyekuwa Mkurugenzi wa Bodi, Mei mwaka jana, akieleza hatari inayoinyemelea bandari kutokana na mfumo wa mawasiliano (Information and Communication Technology – ICT) kuchezewa katika Bandari ya Dar es Salaam na hivyo kupoteza mapato, imani ya wateja na kuhatarisha mizigo inayopitia bandarini.

Kwa mshango wa wengi, Dk. Jabir Bakari aliyeandika barua hii na kutoa ushauri, kwa mizengwe tu kama alivyosema Kipande kwenye kikao kati ya Wakurugenzi wa Bodi na Dk. Mwakyembe, Agosti mwaka jana huko Dodoma, kuwa “yeye ni mteule wa Rais na hivyo wakurugenzi hawambabaishi”, Kipande alifanya mbinu Dk. Jabir akafukuzwa katika Bodi ya Wakurugenzi wa Bandari kwa kutoa ushauri huu. Ifuatayo ni tafsiri isiyo rasmi ya barua hiyo. Endelea…

Kikwete, Warioba wako sawa

Na Christopher Gamaina Wiki iliyopita nchi yetu, Tanzania, iliweka historia ya kipekee. Rais Jakaya Kikwete kwa mara ya kwanza alihutubia wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, ikiwa ni siku mbili baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini,…

Bunge la Katiba livunjwe

Wiki hii Bunge linaanza mjadala wa rasimu ya Katiba. Mjadala huu unafanyika siku chache baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Sinde Warioba, kuwasilisha rasimu hiyo bungeni, na baadaye Rais Jakaya Kikwete naye akalihutubia Bunge. Hotuba mbili za wakubwa hawa ndizo zilizonifanya niandike makala ya leo.

Sitanii, leo tunaumiza vichwa lakini chimbuko la matatizo yote haya liko wazi, ni Rais Jakaya Kikwete. Ibara ya 64 (5) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977) inasema hivi: “Bila ya kuathiri kutumika kwa Katiba ya Zanzibar kwa mujibu wa Katiba hii kuhusu mambo yote ya Tanzania Zanzibar yasiyo mambo ya Muungano, Katiba hii itakuwa na nguvu ya sheria katika Jamhuri nzima ya Muungano na endapo sheria nyingine yoyote itakiuka masharti yaliyomo katika Katiba hii, Katiba ndiyo itakuwa na nguvu, na sheria hiyo nyingine, kwa kiasi inachokiuka Katiba itakuwa batili.”

Ibara ya kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inatoa tangazo la nchi. Inasema Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano. Zanzibar mwaka 2010 walifanya mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar, Ibara ya kwanza ya Katiba ya Zanzibar sasa inasema Zanzibar ni nchi.

Huu ulikuwa ukiukwaji mkubwa wa Katiba ya Tanzania.

Kiwango cha ukiukwaji huu ni sawa na uasi au uhaini.