JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Kipande abanwa Bandari

*Nguvu za ajabu alizokuwa nazo zaanza kuyeyuka, alalamika Kikwete hamsaidii
*Marafiki zake wamtaka asimsingizie Rais, wasema amejiharibia mwenyewe
*Ashinikizwa awarejeshe kazini aliowafukuza kibabe, wafanyakazi washangilia
*Aanza kuogopa kivuli chake, ajitolea ‘photocopy’, adai wanaomsaliti anao TPA
*Mtawa asema asihusishwe na Kipande, bandarini wasema JAMHURI mkombozi
*Mwakyembe aweweseka, adai Lowassa, Profesa Tibaijuka hawamtakii mema
Nguvu za ajabu alizokuwa nazo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Madeni Kipande (58), zimeanza kuyeyuka kwa kasi baada ya GazetiJAMHURI kuchapisha mfululizo maovu anayotenda kwa kutumia wadhifa wake.
Vyanzo vya kuaminika vilivyopo karibu na Kipande, vinasema kwa sasa ameacha kumwamini kila mtu na hasa baada ya JAMHURI kupata habari za ndani ya kikao alichokuwa anatamba kuwa amemng’oa Mkurugenzi wa Masoko, Francisca Muindi, kitu ambacho hakutarajia kuwa kingelifikia gazeti hili.

Yah: Tusichezee lugha yetu, wengine wanajuta

Wakati tunatawaliwa, wakoloni wote kwa awamu zao yaani Wajerumani, Waingereza na hata Wareno na Waarabu, wakati wakipita kwa biashara zao sisi Wazaramo na Wandengereko tulikuwa tunawasiliana kwa shida sana. Kuna wakati tulikuwa tunatumia lugha ya alama kuwasiliana. Baada ya kuanza…

NUKUU

Mwalimu Nyerere: Tudhibiti tofauti za maskini, matajiri “Tofauti kati ya watu maskini na watu matajiri zinaongezeka Tanzania. Inafaa tuwe macho. …lazima tuendelee kutumia Sheria za Nchi, na mipango mbalimbali ya Serikali, kuona kuwa tofauti hizi hazifikii kiasi cha kuhatarisha umoja…

Mwadui ni bora kuliko nyingine nchini – Julio

Kocha wa Timu  ya Soka  ya Mwadui ya mkoani Shinyanga, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, ametamba kwamba timu hiyo itakuwa bora katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara kuliko zote zinazoshiriki.

Akizungumza na JAMHURI hivi karibuni,  Julio amesema kuwa timu hiyo itatoa upinzani mkali kwa timu za Simba,  Yanga  na Azam FC.

“Simba na Yanga hakuna mpira pale bali kuna makelele, niliwahi kufundisha timu ya Kajumulo, sikuwahi kufungwa na Simba wala Yanga na hata sasa nikifanya usajili wangu hakuna timu ya kunifunga kati ya timu hizo,” amesema Julio na kuongeza:

Marijani Rajabu: Jabali la Muziki lililozimika ghafla 

Marijani Rajabu kweli hatunaye tena hapa duniani, lakini kamwe wadau na wapenzi wa muziki wa dansi hapa nchini hawatamsahau.

Alikuwa miongoni mwa wanamuziki waliotoa mchango mkubwa wa maendeleo ya nchi kupitia tungo za nyimbo zake maridhawa, zilizokuwa zikiendana na wakati.

Machi 23, 2014 Marijani alitimiza miaka 18 tangu atangulie mbele ya haki. Nguli huyo alifariki Machi 23, 1995 na kuzikwa siku iliyofuata katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.

Marijani alizaliwa Machi 3, 1955,  Kariakoo, Dar es Salaam. Kwa mapenzi yake Mungu, akamchukua akiwa na umri wa miaka 40.

Hofu yatanda Katiba mpya

*Ananilea: Rais akipenda ataokoa jahazi   Wingu zito limetanda juu ya mchakato wa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya viongozi wa dini na wanaharakati kutabiri kifo chake. Baadhi wamekosoa mfumo wa Bunge Maalum la Katiba, na…