JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Tamisemi yatuhumiwa kuchakachua zabuni

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Jumanne Sagini, anatuhumiwa kutoa zabuni ya uchapaji wa nyaraka za Serikali kwa Kampuni ya Yukos Enterprises Ltd ya mkoani Pwani bila kufuata taratibu.

Viongozi wa dini warejea na matumaini ya maendeleo

Viongozi 19 wa dini mbalimbali hapa nchini kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara, wiki iliyopita wamerejea nchini kutoka katika ziara ya mafunzo nchini Thailand huku wakiwa wamefurahishwa na mafunzo waliyopata.

Mafunzo hayo yalitokana na jitihada za Serikali katika kuhakikisha elimu kuhusu masuala ya gesi asilia na mafuta inatolewa kwa wananchi wa kada mbalimbali, ili kufahamu mchakato mzima wa upatikanaji wa gesi asilia na mafuta.

Pia mafunzo hayo yalilenga kujua faida za gesi katika nyanja za kiuchumi na kijamii, changamoto zake na namna nchi nyingine zinavyotumia rasilimali hiyo katika kukuza uchumi.

Polisi Geita yafyata kwa watuhumiwa

Jeshi la Polisi mkoani Geita limeshindwa kuwakamata walinzi wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo vya ujambazi wa kutumia silaha.

Watuhumiwa hao — Maneno Nangi na John Magige —  wamekwishaapa mbele ya mlalamikaji kwamba wako tayari kutumia fedha zao zote ili kuhakikisha kuwa wanajinasua kwenye tuhuma hizo.

Ukweli kuhusu mabilioni ya IPTL

*Profesa Muhongo, Maswi waanika wanachokiamini

*Wachukizwa wanasiasa kuupotosha umma wa Watanzania

 

 

 

Sakata la Sh bilioni 200 kutoka katika akaunti ya Escrow, inayomilikiwa kwa pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), limeendelea kutawala kwenye mijadala ndani na nje ya Bunge.

Simba imekosea kubeza klabu za Tanzania

Katika hali isiyo ya kawaida, Klabu ya Soka ya Simba imetamba na kuapa kwamba haitathubutu kuwauza hata kwa dau kubwa kiasi gani, wachezaji wake, Amissi Tambwe na Jonas Mkude, kwa klabu yoyote ya hapa Tanzania.

Kwa Nyalandu ni fedha na mamlaka, basi!

Rais Jakaya Kikwete ametangaza Tume ya Kimahakama kuchunguza sakata la Operesheni Tokomeza. Tume inaongozwa na Jaji Hamis Msumi.

Katika kitabu chake cha Uhuru wa Mahakama, Jaji Barnabas Samatta amenukuu sifa kadha wa kadha za mtu anayepaswa kuwa jaji.