JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Tukatae ukatili dhidi ya albino (2)

Juma lililopita nilizungumzia chimbuko na dhana potofu zinazoendelea miongoni mwa jamii yetu kuhusu watu wenye ualbino.  Leo naangalia masuala ya utu, afya, haki, matatizo na usalama wao.

“Watu wenye ualbino” kama wanavyotaka wao wenyewe kuitwa, na wasiitwe albino au zeruzeru kwa sababu majina hayo yanadhalilisha utu wao. Binafsi sioni kama kuna udhalilishaji juu yao.

Maneno hayo mawili ya Kiswahili na Kiingereza yote yanatoa maana ile ile moja ya kukosa rangi kamili ya mwili. Ni vyema ndugu zangu wayakubali majina hayo. Nasema ninawaomba wayakubali majina hayo.

Ugaidi Kenya utuimarishe kiulinzi

 

Wimbi la matukio yanayohusishwa na ugaidi limeendelea kuitesa nchi ya Kenya kwa kuua na kujeruhi watu, kuharibu mali mbalimbali na kuisababishia hasara kubwa.

Wiki iliyopita watu zaidi ya 10 waliripotiwa kuuawa na wengine zaidi ya 70 kujeruhiwa wakati wa milipuko miwili iliyotokea katika soko kubwa la nguo la Gikomba mjini Nairobi.

Huo ni mfululizo wa matukio kadhaa yanayohusishwa moja kwa moja na ugaidi likiwamo lililoshambulia kituo cha maduka ya kifahari cha Westgate jijini Nairobi.

Njama za kumfuta Nyerere hazitafanikiwa

Aprili 22, mwaka huu, katika safu hii nilihoji waliko “Friends of Nyerere”.

Nilifikia hatua ya kuhoji baada ya kasi ya matusi dhidi yake kuongezeka. Matusi hayo kama ilivyotarajiwa, yakaunganishwa hadi kwa Mwasisi wa Zanzibar, Sheikh Abeid Amani Karume.

Waliosikiliza hotuba ya Mjumbe wa Bunge la Katiba, Tundu Lissu, wanajua kinachosemwa. Lakini wapo waliokomaa wakitaka matusi hayo tuyarejee ili wayapime kubaini kama kweli yanastahili kuitwa matusi au ni ukosoaji tu wa kawaida dhidi ya Mwalimu Nyerere na Sheikh Karume.

Kilio cha barabara Dar-Lindi

Mvua za mwaka huu zimetuathiri kiuchumi sisi Watanzania. Mafuriko yametokea karibu katika kila mkoa na kusababisha uharibifu mkubwa katika miundo mbinu ya nchi hii.

Kuna madaraja yamekatika au kumeguka au hata kusombwa na maji kabisa. Haya yametokea katika Barabara ya Dar es Salaam-Bagamoyo pale kwenye Mto Mpiji, barabara ya Dar es Salaam-Kilwa kule Kongowe penye Mto Mzinga.

Aidha, mito kadhaa imefurika na kukata mawasiliano katika maeneo ya Mto Kilombero kule Ifakara, yamekata kivuko kile cha kuunganisha Ifakara na Mahenge. Huko Kyela, vijiji kadhaa vimesombwa na mafuriko. Kilosa eneo la Dumila barabara na daraja yamekwenda na maji. Kule Godegode, reli imeng’olewa na hata hii Barabara Kuu ya Dar es Salaam-Morogoro penye Mto Ruvu, mto umefurika kiasi cha maji kupita juu ya barabara ya lami.

Yah: Tuheshimu, tuthamini kazi tunazopewa

Mara nyingi huwa najaribu kufanya tathmini yangu ya kazi ambazo natakiwa kuzifanya kutokana na kuaminiwa na wenzangu, inaweza ikawa ushenga, ushereheshaji, kufanya utambulisho, kusoma hotuba au risala na kadhalika.

Inapotokea ukapewa heshima hiyo, unatakiwa kuheshimu kazi na kuwaheshimu waliokupatia kazi, unatakiwa kujali na kuthamini heshima hiyo kwa nafasi hiyo uliyopewa kwa imani ya waliokuteua. 
Nakumbuka zamani ilikuwa tunafanya uchaguzi wa viongozi wetu kwa kuangalia hekima, busara na kujituma kwa mtu mwenyewe, vigezo vya shule havikuwa na maana sana kwa sababu hatukuamini kuwa shule peke yake ingeweza kukidhi haja ya busara, heshima na hekima. 

Serikali izitendee haki shule zake

Kama tujuavyo nchini Tanzania kuna shule za aina mbili: Shule za Serikali (ambazo pia huitwa shule za umma) na shule za watu binafsi.

Katika Tanzania ya leo, shule za Serikali ni nyingi zaidi kuliko shule za watu binafsi. Hali haikuwa hivyo wakati wa ukoloni na katika miaka ya mwanzo ya Uhuru. Wakati huo shule za watu binafsi zilikuwa nyingi zaidi kuliko za Serikali.