JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Tuvunje Bunge la Katiba tukawahoji wananchi kama wanataka Muungano

Wiki hii nafahamu kuwa kuna tukio la aina yake nchini. Ni kwa mantiki hiyo, nashindwa kuendelea na mada yangu ya gesi. Naomba niisogeze mbele kwa wiki moja. Yanayotokea ni ya mpito, ila Tanzania itabaki.

Ijue historia ya Kombe la Dunia

Katika kipindi hiki cha kuelekea fainali za soka za Kombe la Dunia zitakazofanyika nchini Brazil kuanzia Juni 12, mwaka huu, JAMHURI imeona vema kuwakumbusha mashabiki, wapenzi na wadau wa soka kwa jumla, historia ya mashindano hayo.

MANU DIBANGO: Gwiji la saxophone lililotimiza miaka 80

Manu Dibango ni gwiji wa kupuliza chombo adhimu katika ulimwengu wa muziki, kilichobatizwa kwa jina la ‘midomo ya bata’ (saxophone) na watu wa ‘mujini’, aliyejizolea sifa kemkem barani Afrika na ulimwenguni kwa ujumla.

Nguli huyo Februari 10, 2014 alitimiza miaka 80 ya kuzalikwa kwake.

Jina lake halisi ni Emmanuel Dibango, ambaye, pamoja na kupuliza saxophone, pia ni mtunzi na mwimbaji mahiri mwenye sauti nzito. 

Biashara ni wateja, tuwajali

Siku moja nilikuwa mji mdogo wa Ilula wilayani Kilolo katika mkoa wa Iringa. Nikiwa hapo niliingia kwenye duka moja la vifaa vya ujenzi nikiwa na lengo la kununua vifaa kadhaa vyenye thamani ya takriban shilingi laki tatu.

Katika duka hilo nilimkuta mama mmoja ambaye wakati akinipokea alionekana kuwa bize kubonyeza simu yake ya kiganjani. Nilipomsalimia hakujibu, na baada ya kuinuka kutoka katika kuitazama simu yake akaniuliza, “Nikusaidie nini?” Mimi nikamjibu kwa kumueleza vifaa ninavyovihitaji na kumuomba anitajie bei zake kimoja kimoja.

GERALD NYAISSA: Kijana msomi anayependa kujiajiri

 

*Hutumia makaburi kumwomba Mungu

Wiki iliyopita JAMHURI ilifanya mahojiano maalum na kijana msomi aliyehitimu elimu ya chuo kikuu katika fani ya utawala wa biashara. Huyu si mwingine yeyote bali ni Gerald Nyaissa, mkazi wa jijini Dar es Salaam.

Mahojiano haya yalijikita zaidi katika suala zima la kuchangamkia fursa za kujiajiri na kujijenga kiuchumi, badala ya kusubiri kuajiriwa serikalini na kupata misaada kutoka kwa wahisani. Yafuatayo ndiyo mahojiano yenyewe:

Rais azibe pengo la wana UKAWA

Kuna haja ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, kuangalia uwezekano wa kuziba pengo lililoachwa wazi na wanachama wa unaoitwa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) katika Bunge Maalum la Katiba.