JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Wenye akili wapo Ikulu!

Rais Jakaya Kikwete alipoamua kuleta suala la Katiba mpya kupitia ilani yake ‘mbadala’, wapo waliomshangaa.

Nakumbuka niliandika makala iliyosema, “Nitakuwa wa mwisho kuishabikia Katiba mpya”. Hiyo haikuwa na maana kwamba sikutambua wala kuthamini matamanio ya Rais wetu kuwaachia Watanzania Katiba nzuri!

KWA HILI LA OKWI Yanga inahadaa mashabiki wake

Edgar Aggaba, mwanasheria wa Emmanuel Okwi, nyota wa soka wa kimataifa kutoka Uganda, hakufika Dar es Salaam kusimamia kesi ya mchezaji huyo wakati Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ilipojadili mkataba na usajili wake katika klabu ya Yanga.

Lovy Longomba Gwiji aliyetokea katika familia ya wanamuziki

“Mtoto wa nyoka ni nyoka.” Usemi huu wa wahenga unajionesha wazi kwa baadhi ya familia zilizojaaliwa kuwa na vipaji vikubwa.

Vipaji hivyo vinaweza kuwa vya kucheza mpira, muziki, kucheza sarakasi, riadha, ndondi n.k.

Warioba, Spika Sitta wateketeza Sh 100bil

MPAKA Jumamosi ya Oktoba 4, mwaka huu, Bunge Maalumu la Katiba Mpya litakuwa limetumia zaidi ya Sh 100 bilioni bila kupatikana kilichotarajiwa.
Fedha hizo, ni hesabu kuanzia Mei mosi, 2012 siku ambayo Tume ya Marekebisho ya Katiba ambayo ilikuwa na kazi ya kukusanya na kuratibu maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya ilipoanza kazi rasmi.

Mchakato wa Katiba haukuandaliwa vizuri

Kama tujuavyo Bunge la Mabadiliko ya Katiba limekumbwa na vurugu na misukosuko kiasi cha kutia aibu Taifa letu.

Nashindwa kusema Bunge hilo liliendelea kujadili Rasimu ya Katiba kwa ukaidi wa nani. Maana wakati wote magenge mbalimbali  ya watu waliendelea kudai Bunge hilo lisitishe shughuli zake, hasa baada ya wabunge wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kususia Bunge hilo.

ongezi JWTZ kwa kutimiza miaka 50   -2

Juma lililopita, nilitoa pongezi kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kutimiza miaka 50 tangu kuanzishwa Septemba Mosi, 1964.  Ukweli Jeshi hili liliasisiwa baada ya Jeshi la Tanganyika (Tanganyika Rifles-TR)  kuasi Januari  20,1964.