JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: MCHANGANYIKO

Tanzania ijitoe Jumuiya ya Afrika Mashariki?

Katika toleo lililopita la gazeti hili, nilizungumzia hali halisi ya ujirani wa Tanzania na nchi nne nyingine zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki Tanzania.

Nilisisitiza kwamba katika Jumuiya ya Afrika Mashariki Tanzania haina majirani wazuri. Nilitoa mfano wa Kenya ambayo imekuwa ikihujumu Tanzania na kuifanyia mambo ya uhasama yanayodhoofisha umoja na ushirikiano  wa Afrika Mashariki.

Kennedy Ndosi: Kina Ridhiwani wananivutia kuwania ubunge

 

Joto la Uchaguzi Mkuu mwakani, litakalohusisha ngazi ya urais, ubunge na udiwani, limepamba moto. Mmoja wa vijana, ambao wanaelekea moja kwa moja kuhitaji kulitumikia Taifa kisiasa ni Kennedy Elimeleck Ndosi, mtaalamu wa Ununuzi na Ugavi. Sifa kubwa ya Ndosi ni kutokukubali kushindwa kwa urahisi. Ni mpambanaji. Hii ni kwa sababu mtaalamu huyo wa ununuzi na ugavi ni mchapakazi. Ndosi ana ndoto za kuwa mbunge, na katika makala hii anajibu maswali katika mahojiano na mwandishi wa makala hii yaliyofanyika ofisini kwake, jijini Dar es Salaam…

Tibaijuka: Nawapigania wasichana

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, ameweka hadharani misaada na michango anayokusanya kwa ajili ya kuwakomboa watoto wa kike.

Ninachokumbuka kuhusu mradi wa maji Ziwa Victoria

Katika dunia kuna mambo yakitokea unajiuliza kwa nini yametokea. Unajiuliza ni hivi hivi au kuna msukumo, ila yote kwa yote nimejiwekea utaratibu wa kusimamia ukweli. Mara zote naamini ukweli unamweka mwanadamu huru, na hapa leo kama nifanyavyo siku zote nitajaribu kueleza ukweli ninaoufahamu.

Malengo ya kazi (2)

Lazima wahakikishe kwamba kazi zote zinaendeshwa barabara, na pamba ya aina itakiwayo inapatikana na wakati ule ule inapoatakiwa; wahakikishe kwamba hakuna kipingamizi  kutoka hatua moja hata nyingine; kwamba kuna uhusiano baina ya kazi mbalimbali, na kwa sababu hiyo hakuna mfanyakazi anayekaa bure kungojea mwenzake amalize kazi yake.

Wakubwa wa kazi hawana budi kuhakikisha kwamba wananunua pamba ya kutosha, na kwamba wana mahali pa kuuzia nguo  zinazotengezwa; kwamba mishahara inalipwa bila ya kuchelewa;  kwamba hesabu ya fedha zinazowekwa sawa sawa; kwamba mitambo inakaguliwa ipasavyo; na mambo mengine kadha.

Tugeukie mabadiliko ya Katiba, maandamano tuwe macho

 

Kumbukumbu zinanionesha sasa kuwa Watanzania wengi wanaamini kuwa suala la Katiba Mpya haliwezekani tena chini ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete. Ametafuta pa kutokea na kuamua kuelewana na wapinzani kupitia Kituo cha Demokrasia (TCD) na wakubwa hawa wakakubaliana yafanyike mabadiliko ya 15 ya Katiba.