Rais wa Marekani Joe Biden amesema kuwa haungi mkono shambulio katika maeneo ya nyuklia ya Iran kufuatia mashambulizi ya makombora ya masafa ya Iran dhidi ya Israel na kuitaka Israel kuchukua hatua ” sawia” dhidi ya adui yake mkuu wa kikanda.

Kauli za Biden siku ya Jumatano zilikuja siku moja baada ya Iran kurusha makombora zaidi ya 180 ya masafa marefu dhidi ya Israeli siku ya Jumanne, katika hatua ambayo Biden aliitaja kuwa “isiyofaa.”

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu aliapa kuwa Iran italipa gharama ya shambulio hilo.

Biden aliwaambia waandishi wa habari kabla ya kupanda ndege ya raias,b Air Force One, “Tutajadiliana na Waisraeli watafanya nini, lakini sisi sote (nchi za G7) tunakubali kwamba wana haki ya kujibu, lakini lazima iwe kwa uwiano.”

Katika miezi ya mwisho ya muhula wake, Biden anakabiliwa na ukosoaji mkali ndani na nje ya nchi kutokana na uungwaji mkono mkubwa wa kijeshi wa Marekani kwa Israel, ukosoaji uleule anaokabiliana nao naibu wake, Kamla Harris, mgombea urais wa Chama cha democrat.

Please follow and like us:
Pin Share