JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Author: Jamhuri

Uamuzi wa kinafiki unaimaliza CCM

Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CC-CCM), mwishoni mwa wiki iliyopita, imetangaza rasmi kumalizika kwa adhabu dhidi ya wanachama wake sita waliodaiwa kufanya kampeni za urais kabla ya wakati.  Uamuzi huo wa Kamati Kuu ya chama hicho ulitolewa na Katibu…

Hatma ya Tanzania iko kwa Jaji Lubuva

Waliosoma maandishi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa zamani, Jaji Mark Bomani, watakubaliana na mawazo yake. Hoja yake kuu ni kwamba Katiba mpya katika mazingira ya sasa ya nchi yetu, haiwezekani. Kwa maana hiyo hatuwezi kuwa na Uchaguzi Mkuu mwaka…

Yah: Laana yangu kwa hawa, baraka kwa wale

Sasa niseme rasmi kuwa mimi nakubali siasa ya Ujamaa na Kujitegemea kuwa nguzo yetu ya kujitegemea na kututoa hapa tulipo na kutupeleka katika nchi ya ahadi ya kunywa maziwa na asali, nchi ya ahadi ya Eden ambayo kwa hakika ndiyo…

Salaam wafanyakazi wote

Itakumbukwa katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, Mei mosi mwaka huu, iliyofanyika kitaifa Uwanja wa Michezo CCM Kirumba, Mwanza, yalionekana na kusikika mambo mengi ikiwamo michezo, ngoma na nyimbo zilizosifu na kushauri utendaji bora wa kazi na kudumisha nidhamu ya…

CCM ina nia mbaya kwa makada wake?

Baada ya danadana ya muda mrefu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inayoendelea kukwamisha kumtangaza mgombea wao wa urais, sasa naamua kusema. Hii ni kwa sababu ni mwanachama wa kawaida na sina nafasi ndani ya vikao vya Kamati Kuu wala Halmashauri…

Sababu nne za ushahidi wa kuambiwa haukubaliki kortini

Ushahidi wa kuambiwa ni nini? Ushahidi wa kuambiwa ni ule unaotolewa na mtu ambaye hakuona tukio likitendeka, hakusikia tukio likitendeka, hakuhisi wala kuonja, wala kunusa jambo lililo mbele ya Mahakama kama kosa isipokuwa aliambiwa na mtu mwingine aliyeona, kusikia, kuhisi,…