Takriban watu 50 wamefariki baada ya boti iliyokuwa imewabeba kupinduka katika Ziwa Kivu, mashariki mwa Kongo hii leo.Mashuhuda wameliambia shirika la habari la AP.

Idadi kamili ya waliokuwamo kwenye boti hiyo haikufahamika mara moja na kwamba ni watu watu wangapi waliokuwemo ndani ya boti hiyo na ni wangapi ambao wameangamia.

Mashuhuda wamesema watoa huduma ya uokozi walisaidia kutoa miili 50 kwenye maji huku watu 10 wakinusurika na kupelekwa katika hospitali ya mtaa.

Please follow and like us:
Pin Share