Mwanzilishi wa mtandao wa Telegram Pavel Durov, amepelekwa mahakamani mjini Paris ambapo anaweza kufunguliwa mashtaka rasmi, baada ya muda wa kwanza wa kukamatwa na kuhojiwa kumalizika.

Mwanzilishi wa mtandao wa Telegram Pavel Durov, amepelekwa mahakamani mjini Paris ambapo anaweza kufunguliwa mashtaka rasmi, baada ya muda wa kwanza wa kukamatwa na kuhojiwa kumalizika.Telegram yamkamatisha mtuhumiwa ugaidi Ujerumani

Mwanzilishi huyo ambaye ni Mrusi mwenye umri wa miaka 39 alikamatwa kwenye uwanja wa ndege wa Le Bourget, katika mji mkuu wa Ufaransa Jumamosi iliyopita kwa tuhuma za kushindwa kuchukua hatua kudhibiti maudhui hasi kwenye mtandao wake wa kijamii unaotumiwa na watu milioni 900. Kampuni ya Telegram imeyekanusha madai hayo.

Hata hivyo, hatua ya kuwekwa chini ya uchunguzi rasmi nchini Ufaransa hakuna maana ya kutiwa hatiani ingawa uchunguzi huo unaweza kuchukua miaka kadhaa.

Please follow and like us:
Pin Share