Na James Mwanamyoto (OR-TAMISEMI)

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Deogratius Ndejembi amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa shilingi milioni 331 kupitia mradi wa BOOST zilizojenga madarasa yatakayotatua changamoto ya msongamano wa wanafunzi katika shule ya Msingi ya Mambamba ‘B’ Wilayani Tandahimba.

Ndejembi amesema hayo akiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba, mara baada ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa kumpatia fursa ya kuzungumza na wakazi wa eneo hilo. 

Ndejembi amefafanua kuwa, Rais wa Awamu ya Sita Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alitafuta zaidi ya bilioni 230 kwa ajili ya kujenga shule mpya na madarasa nchi nzima kupitia Mradi wa BOOST kwenye maeneo ambayo shule zina msongamano wa wanafunzi au hakuna shule, ambapo Tandahimba imenufaika na ujenzi wa shule ya Msingi ya Mambamba ‘B’ iliyogharimu milioni 331.

“ Waziri Mkuu milioni 331 imejenga madarasa haya mazuri yenye kupendeza katika Shule hii ya Msingi ya Mambamba ‘B’ ambayo yatasaidia kutatua changamoto ya msongamano wa wanafunzi uliopo katika shule mama ya Mambamba, ikiwa ni pamoja na kuwaondolea hadha wanafunzi kutembea umbali mrefu,” Mhe. Ndejembi amesisitiza.

Ameongeza kuwa, Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imepokea milioni 95 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu wa shule ya msingi na milioni 95 nyingine kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu wa shule za sekondari.

Aidha, Ndejembi amesema TARURA imetenga fedha kwa ajili ya kukarabati barabara ya Kilomita 7.2 ya kutoka Mambamba kwenda Mwimbi hadi Tandahimba ili iweze kupitika katika majira yote.

……………………………………………………………………………


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi wa Mambamba Tandahimba kabla ya kumpatia fursa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Deogratius Ndejembi   kuzungumza na wananchi wa eneo hilo.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na wananchi wa Mambamba Tandahimba alipopatiwa fursa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa kuzungumza na wananchi hao.

Wananchi wa Tandahimba wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Deogratius Ndejembi (hayupo pichani) alipopewa fursa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa kuzungumza nao
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akijadiliana jambo na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Deogratius Ndejembi   kabla ya kuzungumza na wananchi wa Mambamba Wilayani Tandahimba

.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akielekea kukagua miundombinu ya elimu inayojengwa na Serikali katika Shule ya Msingi Mambamba ‘B’ kupitia mradi wa BOOST

.

Mwonekano wa madarasa ya Shule ya Msingi Mambamba ‘B’ yaliyojengwa na Serikali kupitia mradi wa BOOST.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa Serikali mara baada ya kuwasili Mambamba Tandahimba kukagua miundombinu ya elimu inayojengwa kupitia mradi wa BOOST katika Shule ya Msingi Mambamba ‘B’

Please follow and like us:
Pin Share