JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Year: 2024

Klabu ya waandishi wa Habari Dar es Salaam, Polisi Kanda Maalum waunda kamati shirikishi

Na Mwandishi Wetu, JamhuriMedia, Dar es Salaam WAANDISHI wa habari na askari Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam wameshauriwa kutenda kazi kwa kuheshimu misingi ya kisheria, haki za binadamu, utu wa mtu, haki za watu na haki za msingi…

Bashungwa : Wahandisi washauri wababaishaji wachukuliwe hatua kali za kisheria

Na Mwamvua Mwinyi, Pwani Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameagiza kuchukuliwa hatua kali za kisheria kwa wahandisi washauri wababaishaji ambao wameshindwa kusimamia miradi ya ujenzi wa barabara na kupelekea kuharibika kabla ya wakati. Ameeleza, wahandisi hao wamekuwa wakiisababishia hasara kubwa…

Mabula: Mkataba hautaongezwa ujenzi soko la Tarime

Na Helena Magabe Jamhuri media Tarime Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya hesabu za Serikali za mitaa (LAAC), Stanslaus Mabula ameagiza Halmashauri kusimamia mradi wa soko na itakapofika Mei 17,2024 ujenzi uwe umeisha. Ameiomba Halmashauri hiyo kuipatia…

Majaliwa azitaka halmashauri kuweka mpango wa ufuatiliaji na tathmini ya matumizi ya ardhi

Na Mwandishi Wetu, JakhuriMedia, Lindi WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amezielekeza Halmashauri zote zinazotekeleza mradi wa Mpango wa Matumizi ya Ardhi ya Vijiji kuandaa mpango wa ufuatiliaji na tathmini ili kupima ufanisi wa utekelezaji wa mradi huo. Ametoa maelekezo hayo leo…

Bila ya amani, hakuna mtangamano na maendeleo

Nchi Wanachama za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) zimetakiwa kufanya kila linalowezekana kuhakikisha kuwa nchi zao zinakuwa na amani, Umoja na utulivu na kutafuta ufumbuzi wa migogoro kwa kutumia njia zao wenyewe. Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Mkutano…

Mbaroni kwa kumuua mkewe na kumzika chumbani

Na Mwandishi Wetu, JamhuriMedia, Morogoro Jeshi la Polisi mkoani Morogoro  linamshikilia mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la  Mohamedi Omari, mkazi wa kijiji cha Kimamba A, wilayani  Kilosa  kwa tuhuma za  kumuua mkewe  na kumzika ndani ya chumba wanacholala. Tukio hilo la…